Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNGA78

MKUTANO WA 78 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Pata habari kutoka UNGA78

Jukwaa  limeandaliwa kwa ajili ya mjadala mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Wakati ulimwengu ukiendelea kukabiliwa na mdororo wa kijamii na kiuchumi kutokana na Covid 19 na athari zinazoendelea za vita nchini Ukraine, mjadala utafanyika kikamlifu ana kwa ana kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2019, na viongozi wa ulimwengu wakielekea NY kuwasilisha kauli zao katika Ukumbi mashuhuri. 

Hapa, Habari za UN inakupa kiti cha mstari wa mbele katika shughuli zote. Katika simu yako ya mkononi au kompyuta, fuatilia Wakuu wa Nchi na Serikali wanapofafanua hatua dhidi ya changamoto kubwa zaidi duniani na kushiriki katika majadiliano ya ngazi ya juu kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), hatua kabambe ya kumaliza janga la tabianchi, na vikao vitatu vya ngazi ya juu visivyo na kifani kuhusu afya: maandalizi dhidi ya majangahuduma ya afya kwa wote; na mapambano ya kimataifa dhidi ya kifua kikuu

Tutembelee kwenye majukwaa yetu ya mtandao wa kijamii

Twitter: twitter.com/HabarizaUN

Youtube: https://www.youtube.com/@UNNewsKiswahili 

Mkutano wa Kilele wa Wakati UjaoZama zijazo ambao Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa umealikwa unatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 22-23 Septemba.
UN Photo/Laura Jarriel

Septemba 22 hadi 30 Wiki ya ngazi za juu katika UN: Ni nini kinaendelea ulimwenguni na zama zijazo?

Ni msimu wa kushughulikia changamoto za kimataifa, kuanzia kujenga sayari yenye afya hadi kusimamisha ueneaji wa silaha za nyuklia. Viongozi wa dunia na wataalamu watakutana katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, New York, katikati ya mwezi Septemba, kwa ajili ya Wiki ya ngazi za Juu ya Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ili kuweka njia kuelekea mustakabali bora, salama, na kijani kwa wote. Wiki hiyo itakapoanza kutoka tarehe 22 hadi 30 Septemba, haya ndiyo unayohitaji kujua:

UN News/Assumpta Massoi

Vijana tusiwe watazamaji bali tuchukue hatua kwa kuanza na tulicho nacho- Emmanuel

Vijana wana dhima kubwa katika kusongesha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs yanayofikia ukomo mwaka 2030. Mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa kutambua nafasi hiyo ya vijana wanatumia vijana wenyewe ili wawe mabalozi wa mashirika hayo mashinani ili kupigia chepuo yale yaliyomo kwenye SDGs. Mathalani nchini Tanzania shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF lina mabalozi na miongoni mwao ni Emmanuel Cosmas Msoka yeye akijikita kwenye masuala ya usafi wa maji, usafi wa mazingira (WASH) na ubunifu.

Sauti
3'33"
UN News

Tanzania tumepiga hatua kubwa kupambana na kifua kikuu: Waziri Ummy Mwalimu

Kifua kikuu au TB ni moja ya changamoto kubwa za kiafya duniani na janga ni kubwa zaidi Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO duniani kote, TB ni sababu ya 13 inayoongoza kwa vifo na ya pili muuaji wa magonjwa ya kuambukiza baada ya COVID-19 ikiwa juu ya VVU na Ukimwi. Shirika hilo linakadiria kwamba mwaka 2021, takriban watu milioni 10.6 waliugua kifua kikuu kote duniani wakiwemo wanaume milioni sita, wanawake milioni 3.4 na watoto milioni 1.2.

Sauti
3'39"
Rais wa Baraza Kuu la UN Balozi Dennis Francis akiwapatia waandishi wa habari tathmini ya vikao vya ngazi ya juu vya mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la UN (UNGA78).
UN /Eskinder Debebe

SDGs zilikuwa 'mdomoni' mwa kila mtoa hotuba – Rais UNGA78

Kile nilichoshuhudia ni jamii ya kimataifa iliyojizatiti upya kukamilisha utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ifikapo mwaka 2030, amesema Rais wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA78, Dennis Francis akizungumza na waandishi wa habari, ikiwa ni mara ya kwanza tangu ashike wadhifa huo.