UN Women: Vita nchini Sudan vimegeuka kuwa vita dhidi ya wanawake
Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake (UN Women) limetoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka kukomesha ukatili na mateso yanayowakumba wanawake na wasichana nchini Sudan, likisema kuwa vita vinavyoendelea vimegeuka kuwa “vita dhidi ya wanawake.”