Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Msukumo dhidi ya TB ufanane na ule wa COVID-19- Waziri Wafula

Msukumo dhidi ya TB ufanane na ule wa COVID-19- Waziri Wafula

Pakua

Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mapambano dhidi ya Kifua Kikuu au TB ukifanyika leo hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani, Waziri wa Afya wa Kenya Susan Nakhumicha Wafula amesema kutokomeza TB ifikapo mwaka 2030 inawezekana endapo dunia itashikamana na kuweka msokumo mkubwa kwa ugonjwa huo kama ilivyofanya wakati wa mlipuko wa janga la COVID-19. Waziri Wafula alizungumza na Flora Nducha wa Idhaa  hii ya Umoja wa Mataifa.

Audio Duration
8'40"
Photo Credit
UN News