Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNGA78

MKUTANO WA 78 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Pata habari kutoka UNGA78

Jukwaa  limeandaliwa kwa ajili ya mjadala mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Wakati ulimwengu ukiendelea kukabiliwa na mdororo wa kijamii na kiuchumi kutokana na Covid 19 na athari zinazoendelea za vita nchini Ukraine, mjadala utafanyika kikamlifu ana kwa ana kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2019, na viongozi wa ulimwengu wakielekea NY kuwasilisha kauli zao katika Ukumbi mashuhuri. 

Hapa, Habari za UN inakupa kiti cha mstari wa mbele katika shughuli zote. Katika simu yako ya mkononi au kompyuta, fuatilia Wakuu wa Nchi na Serikali wanapofafanua hatua dhidi ya changamoto kubwa zaidi duniani na kushiriki katika majadiliano ya ngazi ya juu kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), hatua kabambe ya kumaliza janga la tabianchi, na vikao vitatu vya ngazi ya juu visivyo na kifani kuhusu afya: maandalizi dhidi ya majangahuduma ya afya kwa wote; na mapambano ya kimataifa dhidi ya kifua kikuu

Tutembelee kwenye majukwaa yetu ya mtandao wa kijamii

Twitter: twitter.com/HabarizaUN

Youtube: https://www.youtube.com/@UNNewsKiswahili 

Waziri wa mambo ya nje wa India, Subramaniam Jaishankar, akihutubia kikao cha 78 cha mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
UN Photo/Cia Pak

Katika enzi zilizoghubikwa na ubaguzi, mizozo na migawanyiko, diplomasia ndio suluhu pekee ya ufanisi: India

Waziri wa mambo ya nje wa India, Subramaniam Jaishankar, akihutubia kikao cha 78 cha mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo amesema kuwa katika wakati ambapo dunia inapitia misukosuko isiyo na kifani kuanzia mgawanyiko kati ya ulimwengu wa Mashariki na Magharibi unaoongezeka, na mvutano wa kimataifa baina ya Ulimwengu wa Kaskazini na Kusini kuzidi kuongezeka, diplomasia na mazungumzo ndio suluhisho pekee la ufanisi la kukabiliana na changamoto za sasa.