Makala Maalum

Kabla ya kukata msaada hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na magonjwa zichukuliwe:Lowcock

 Akitafakari miaka miine ya uongozi wake kama mratibu mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa na mkuu wa OCHA, Mark Lowcok amesema ni jinsi gani watu zaidi na zaidi wanavyohitaji msaada wa kibinadamu kwa sababu ya vita, mabadiliko ya tabianchi na magonjwa kama mlipuko wa Ebola na janga la corona au COVID-19.

Mwendesha Mashtaka Mkuu Mpya wa ICC aapishwa Rasmi

“Naapa kwamba nitatekeleza majukumu yangu kwa Mamlaka yangu ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Kamosa ya Jinai kwa heshima, uaminifu, bila upendeleo na kwa dhamiri, nitaheshimu usiri kwenye kufanya uchunguzi na kuendesha mashtaka” kiapo cha Mkuu mpya wa ICC

 

Punguzeni Gharama ya utumaji fedha:Guterres

“Nawasihi wadau wote kuendelea na juhudi za kupunguza gharama za kuhamisha fedha duniani, gharama hizo zipungue na hata zikaribia sifuri, maana hii ni huduma muhimu sana, hasa kwa nchi zinazoendelea.”

Asilimia 99 ya Watoto Niger hawajui kusoma na kuandika:Benki ya Dunia

Ikiwa leo ni siku ya mtoto wa Afrika, ndoto za kutimiza ajenda ya bara hilo ya mwaka 2040 ya kuwa na bara la Afrika linalomfaa mtoto wa Afrika ikiwemo katika suala la kupata elimu, kwa Niger huenda lisitimie kwani asilimia 99 ya watoto wenye umri wa miaka 10 ni wajinga wa kutokujua kusoma na kuandika.

 

Dola Milioni 135 zatolewa na UN kusaidia wanaokabiliwa na Njaa

Umoja wa Mataifa umetoa dola milioni 135 kutoka kwenye Mfuko wake wa dharura (CERF) ili kuongezea kwenye shughuli za kibinaadamu katika nchi 12 barani Afrika, Amerika na Mashariki ya Kati, amesema Mratibu wa Mfuko huo Bwana Mark Lowcock akiwa mjini New York, Marekani.

 

UN imelaani vikali shambulio la kutisha hospitali nchini Syria

 Maafisa wakuu wa Umoja wa Mataifa leo wamelaani vikali shambulio baya lililofanyika katika hospitali nchini Syria mwishoni mwa wiki na kusisitiza haja ya uwajibikaji kwa uhalifu uliofanywa katika vita vya miaka kumi vya nchi hiyo. 
 

UN yalaani mauaji ya mjamzito nchini Palestina

Umoja wa Mataifa umelaani vikali mauaji ya mwanamke mjamzito mwenye umri wa miaka 19 aliyeuwawa na mume wake nchini Palestina, na kutoa wito vya vyombo vya usalama vya nchi hiyo kuhakikisha haki inatendeka
 

Watoto 33,000 hatarini kufa nchini Ethiopia- UNICEF

Takriban watoto 33,000 katika eneo ambalo halifikiki la Tigray nchini Ethiopia wana utapiamlo mkali na wanakabiliwa na vifo iwapo msaada wa haraka hautapatikana, imesema taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF Henrietta Fore iliyotolewa leo jijini New York, Marekani. 
 
 

Nchi mbili za Afrika zachaguliwa kuingia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa

Nchi za Ghana na Gabon kutoka Afrika zimechaguliwa hii leo kuingia kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa miaka miwili kuanzia januari 1, 2022 pamoja na nchi nyingine tatu. 
 

IRAQ yashauriwa kutoa kipaumbele kwa makundi hatarishi

Ripoti mpya mbili zilizotolewa na Umoja wa Mataifa zimesema lazima kipaumbele kitolewe katika mikakati ya kujikwamua na janga la corona au COVID-19 kwa makundi yaliyo hatarini nchini Iraq wakiwemo wanawake, vijana na wakimbizi wa ndani ili kuhakikisha ujumuishwaji na uendelevu katika kujikwamua huko.