Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Vizuizini nchini Ufilipino ni miongoni mwa vilivyo na watu wengi zaidi duniani.
UNODC/Laura Gil

Kanuni za Nelson Mandela zachukua sehemu muhimu katika marekebisho ya adhabu nchini Ufilipino.

Hali katika vituo vya rumande nchini Ufilipino, ambayo imeelezwa kuwa “si ya kibinadamu” na mmoja wa majaji wa mahakama ya juu nchini humo, inatarajiwa kuboreka kwa kasi wakati taifa hilo la Kusini Mashariki mwa Asia likielekea katika kupitisha sheria zinazozingatia haki za binadamu na utu wa wafungwa na kupendekeza kiwango cha chini cha matibabu katika vituo vyote vya rumande.

Michoro ya sanaa inayoonyesha matumizi ya akili ya bandia.
© IAEA/А. Варгас

IAEA: Maeneo Saba ambayo AI itabadilisha Sayansi na Teknolojia

Katika muongo mmoja uliopita, teknolojia zinazohusiana na akili mnemba maarufu kama AI zimekua upesi zaidi na  zenye uwezo wa kutatua matatizo yanayozidi kuwa magumu. Akili mnemba inatumika katika sekta mbalimbali, kama vile viwanda, usafirishaji, fedha, elimu, na afya. Vile vile, akili mnemba inaweza kuchangia maendeleo ya sayansi ya nyuklia, teknolojia na matumizi yake. Kutumia nguvu za akili mnemba katika uwanja wa nyuklia kunaweza kutoa mchango mkubwa katika kutatua changamoto kubwa zaidi za wakati wetu, kutoka kwa kupambana na mabadiliko ya tabianchi hadi kuhakikisha kuna uhakika wa chakula.

Watoto wakijifunza jinsi ya kupatia chanjo kuku huko Ouahigouya, Burkina Faso.
© UNICEF/Ndiaga Seck

Burkina Faso: Mgogoro uliosahaulika Afrika : Kurejesha elimu bora

Nchini Burkina Faso, ufadhili kutoka Mfuko wa Elimu Haiwezi Kusubiri au Education Cannot Wait, wadau wa elimu duniani likiwemo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF na wadau wa kimkakati wanawarejesha shuleni wasichana na wavulana. Wanarejeshwa maeneo salama wanakoweza kujifunza kwa njia mbali mbali ikiwemo kupitia vipindi vya redio. Wakipatiwa  mafunzo kama ya ufundi ili hatimaye wajifunze kile walichokosa.

Daniel Berruezo mfanyakazi wa wizara ya kazi ya Argentina jimboni Salta
© ILO/Gastón Chedufau

Nilikuwa mwathirika wa ajira ya watoto lakini sasa nafanya kila niwezalo kuizuia: Daniel Berruezo

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kupinga ajira kwa watoto ambayo mwaka huu imebeba maudhui “Hebu tutekeleze ahadi zetu kukomesha ajira ya watoto” tunaelekea nchini Argentina kukutana na muathirika wa ajira ya watoto ambaye sasa  ameamua kulivalia njuga suala hilo na anafanya juu chini kuitokomeza ajira kwa watoto ambayo imekita mizizi nchini humo kwa miaka nenda miaka rudi.  

Watu waliokimbia makazi yao mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mara nyingi hukumbwa na mashambulizi ya kiholela huku mapigano yakiendelea kati ya wanajeshi wa serikali na waasi.
UNHCR/S. Modola

DRC dhuluma nyingi dhidi ya watoto Kivu Kaskazini zinafanyika maeneo ya mapigano: UNHCR

Mbali na mauaji, watoto wamekuwa ni waathirika wakubwa wa utekaji nyara, unyanyasaji wa kingono, lakini pia kuandikishwa na kutumiwa na makundi yenye silaha vitani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR likibainisha kuwa dhuluma nyingi dhidi ya watoto hao Kivu Kaskazini hutokea katika maeneo ya mapigano.

Sheij Aldine, mwanachama wa Shirika la Watu Wenye Ulemavu cha Sudan, akiendesha pikipiki maalum iliyotolewa na shirika hilo huko Darfur Kaskazini, Sudan.
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Mambo 5 kuhusu Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu

Hebu fikiria maisha ya kila siku bila kuona, kukosa kiungo, au maisha yenye changamoto za kuwa na akili inayofanya kazi tofauti na mtu wa kawaida au kupooza. Huu ni ukweli kwa baadhi ya watu. Kwa mujibu wa Shirika Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO), mwaka 2023, mtu mmoja kati ya sita, sawa na asilimia 16 ya watu wote duniani, walikuwa wanaishi na ulemavu. Wengi wanategemea Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu kuwasaidia kuhifadhi uhuru wao wa kimsingi na heshima yao.