Skip to main content

Chuja:

Makala Maalum

Mradi wa FAO nchini Thailand wa kupunguza upotevu wa chakula na taka kuna jukumu muhimu katika kubadilisha mifumo ya kilimo na chakula.
© FAO/Alisa Suwanrumpha

Mradi wa FAO wa kupunguza upotevu na utupaji wa chakula nchini Thailand wainua kipato cha wafanyabiashara

Kupunguza upotevu na utupaji wa chakula kuna jukumu muhimu katika kubadilisha mifumo ya kilimo na chakula. Kati ya malengo 17 ya Maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ambayo yanafikia kilele mwaka 2030 lengo namba 2 linahimiza kutokomeza njaa, lengo namba 8 linahimiza kazi nzuri na ukuaji wa kiuchumi na lengo namba 12 lina himiza utumiaji na uzalishaji wenye kuwajibika lengo likiwa kuwa na mifumo endelevu ya utumiaji wa rasilimali. Malengo yote haya yanaenda sambamba na harakati za kupunguza upotevu na utupaji wa chakula.

Sio tu kwamba mikoko inasaidia kuzuia kuendelea kwa mabadiliko ya tabianchi, lakini pia ina jukumu muhimu katika kupunguza athari zake.
The Mangrove Photography Awards/Shyjith Kannur

Haya ndiyo mambo ya kutarajia katika Wiki ya mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi barani Afrika 2023

Viongozi wa Afrika wanatarajiwa kukutana jijini Nairobi, kenya wiki ijayo kwa jaili ya wiki ya mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi, Mkutano wa kila mwaka ambao wanatarajiwa kujadili njia mbalimbali za kupunguza utoaji wa gesi chafuzi huku wakija na mbinu za mnepo wa kukabiliana na athari za hali ya hewa.

Amadou Jobe, mhamiaji ambaye alirejea Gambia kutoka Ulaya, akiangalia bahari ya Pasifiki kutoka pwani ya Gambia.
UN News/ Hisae Kawamori

Sitamani tena kuzamia kwenda Ulaya: Manusura kutoka Gambia

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Afrika hujaribu kufika Ulaya wakivuka bahari ya Mediterania kwa lengo la kwenda kusaka maisha bora lakini safari hiyo inaelezwa kuwa ni hatari sana kwani maelfu ya watu hufa maji au kutoweka. Evariste Mapesa anatupeleka nchini Gambia kusikia simulizi ya kijana ambaye chupuchupu apoteze maisha. 

 

Sauti
3'19"
Kina mama kutoka Kenya ambao wananyonyesha watoto wao, wakiwatumbuiza wageni kwenye uzinduzi wa wiki ya kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa kunyonyesha.
UN News/Thelmaa Mwadzaya

Unyonyeshaji wa watoto maziwa ya mama huimarisha afya yao na ya mama - Wanaharakati Kenya

Kulingana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, watoto wanaonyonya maziwa ya mama pekee katika miezi sita ya mwanzo ya uhai wanapiga hatua nzuri za kiafya kama anavyoelezea Kasha Mutenyo kwamba, "umuhimu wa kwanza wa kunyonyesha ni kwamba afya ya mtoto inaimarika na haugui kila wakati. Sio ghali, ni salama na hauhitaji vifaa vyovyote kumnyonyesha mtoto. Pia inamsaidia mama kupanga uzazi.”

Sauti
6'58"