Kila mwaka tarehe 29, mwezi wa Mei Umoja wa mataifa huadhimisha siku ya walinda amani duniani, na leo hapa kwenye makao makuu imefanyika hafla maalum ya kuadhimisha siku hiyo muhimu ya kukumbuka mchango wa walinda amani duniani, ambao ni wake kwa waume wanaohudumu kama wanajeshi, polisi ama raia kwenye majukumu ya ulinzi wa amani.