Miaka minne ya utumishi wa Joyce Msuya ndani ya UNOCHA
Joyce Msuya, Naibu Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada ya dharura, OCHA anatamatisha jukumu lake baada ya kuhudumu kwa miaka minne. Ndani ya muda huo wa uongozi wake ametembelea zaidi ya nchi 30 na amekuwa akizungumza na watu katika shida na matumaini, umefanya takribani mikutano 20 na wanafunzi katika nchi mbalimbali na alipokuwa akirejea Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani aliongea na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zaidi ya mara 40 ukiwa ni wastani wa karibia mara moja kila mwezi kueleza yale aliyoshuhudia mashinani pamoja na namna ofisi yake inavyowasadia wananchi. Hizi ni chache kati ya maelfu ya picha zinazoonesha akitekeleza majukumu yake.
Habari Zaidi katika picha
Pagination
- Page 1
- Next page