Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNGA78

MKUTANO WA 78 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Pata habari kutoka UNGA78

Jukwaa  limeandaliwa kwa ajili ya mjadala mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Wakati ulimwengu ukiendelea kukabiliwa na mdororo wa kijamii na kiuchumi kutokana na Covid 19 na athari zinazoendelea za vita nchini Ukraine, mjadala utafanyika kikamlifu ana kwa ana kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2019, na viongozi wa ulimwengu wakielekea NY kuwasilisha kauli zao katika Ukumbi mashuhuri. 

Hapa, Habari za UN inakupa kiti cha mstari wa mbele katika shughuli zote. Katika simu yako ya mkononi au kompyuta, fuatilia Wakuu wa Nchi na Serikali wanapofafanua hatua dhidi ya changamoto kubwa zaidi duniani na kushiriki katika majadiliano ya ngazi ya juu kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), hatua kabambe ya kumaliza janga la tabianchi, na vikao vitatu vya ngazi ya juu visivyo na kifani kuhusu afya: maandalizi dhidi ya majangahuduma ya afya kwa wote; na mapambano ya kimataifa dhidi ya kifua kikuu

Tutembelee kwenye majukwaa yetu ya mtandao wa kijamii

Twitter: twitter.com/HabarizaUN

Youtube: https://www.youtube.com/@UNNewsKiswahili 

Katibu Mkuu António Guterres (Kulia) akihojiwa na Mita Hosalia (Kushoto) Naibu Mkurugenzi wa kitengo cha Habari na Vyombo vya Habari katika idara ya mawasiliano ya Umoja wa Mataifa.
UN Photo/Mark Garten

UNGA78: Mkuu wa UN apuuza kutokuwepo kwa viongozi wakuu, asema lazima ahadi za maendeleo na mabadiliko ya tabianchi zitimizwe

Huku viongozi kadhaa wa ngazi za juu duniani wakijiondoa kwenye kuhudhuria kikao cha ufunguzi cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wiki ijayo, Katibu Mkuu wa Umoja huo António Guterres amesema hajali ni nani anayekuja New York na kikubwa zaidi kwake ni kuhusu nini kifanyike, hasa kufufua hali inayodemadema ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo (SDGs).