Skip to main content

Chuja:

Habari Mpya

Wakimbizi wa Sudan wakielekea nchi jirani.
© WFP/Jacques David

Wakimbizi wa Sudan wengi zaidi nchini CAR, UNHCR yakimbizana na muda kuiwahi mvua  

Zaidi ya watu 13,000 kutoka Sudan wamewasili katika Kijiji cha Am Dafock kaskazini mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati ili kuepuka madhila ya mgogoro unaoendelea nchini mwao. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi linasema wengi wa waliowasili ni wanawake na watoto kutoka Nyala mji ulioko kusini magharibi mwa Sudan ambako wanasema walikabiliwa na matatizo kadhaa njiani kuelekea kuvuka mpaka hadi kufika Am Dafock, kama vile vitisho kutoka kwa watu wenye silaha, unyang'anyi wa bidhaa, unyanyasaji wa kimwili na unyanyasaji wa kijinsia. 

Sauti
3'25"
Prime Metal, mnufaika wa mradi wa RAPID IMPACT PROJECT nchini DRC ambaye aliwahi kutekwa nyara na kuokolewa juhudi za MONUSCO .
Byobe Malenga/UN News

Nilitekwa nyara na waasi, lakini MONUSCO ilinikomboa- Mwananchi DRC 

Wiki hii dunia imeadhimisha miaka 75 tangu kuanzishwa kwa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa mwaka 1948. Tangu mwaka huo zaidi ya wafanyakazi milioni mbili waliovalia sare kijeshi na raia wamesaidia nchi kuhama kutoka vita hadi kwenye amani. Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umekuweko tangu mwaka 2000, ikimaanisha mwaka huu ni miaka 23.

Walinda amani wa Umoja wa MAtaifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO wamesherehekea siku ya walinda amani duniani kwa kutembelea kituo cha watoto yatima huko Oicha jimboni Kivu Kaskazini.
UN News/George Musubao

DRC: Walinda amani wa UN kutoka Tanzania washerehekea siku yao kwa kutembelea watoto

Kikosi cha 10 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANZBATT-10 kinachohudumu kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi (FIB) kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kimeadhimisha siku ya ulinzi wa amani duniani hii leo tarehe 29 Mei kwa kutembelea kituo cha watoto yatima cha DORIKA kilichopo OICHA Jimbo la Kivu kaskazini nchini DRC. Wakiwa kituoni hapo wamewapatia misaada ya kiutu watoto hao ikiwa pia ni lengo la kulinda uhusiano na ushirikiano kwenye eneo lao hilo la uwajibikaji.

Hawaye Ibrahim, mkimbizi wa Sudan nchini Chad, anasema wanamgambo walivamia nyumba yao huko Darfur nchini Sudan ambapo walimuua mume wake, wakamjeruhi mtoto wake huku wakitumia fimbo kumchapa sikio la kushoto na hadi sasa ana maumivu.
UNHCR Video

Simulizi ya mama aliyekumbwa na machungu Sudan

Walimuua mume wangu, walijeruhi mwanangu na mimi walinipiga, ni simulizi ya mama ambaye sasa yuko na watoto wake nchini Chad akitokea Sudan kwani nchini mwake ni kama wasemavyo wahenga, Amkani si shwari kufuatia mapigano yaliyoanza tarehe 15 mwezi Aprili mwaka huu ambayo pamoja na kuua zaidi ya watu 700 wengine zaidi ya 300,000 wamekimbilia nchi jirani ikiwemo Chad na miongoni mwao ni Hawaye Ibrahim.

Sauti
3'18"
Afisa habari wa kikosi Cha sita kapteni mwijage inyoma akipokea zawadi kutoka Kwa Mkuu wa Mkoa wa NOLA baada ya timu ya kikosi Cha TANBAT6 chini ya MINUSCA kupata ushindi wa michezo wa mpira wa miguu kati yake na Gender marine polisi NOLA.
© TANBAT 6

Asante TANBAT6 kwa kuchangia maendeleo yetu: Wananchi CAR

Katika wiki ya kulekea maadhimisho ya siku ya walinda amani duniani kikosi cha sita cha walinda amani kutoka Tanzania TANBAT 6 kinachohudumu chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati MINUSCA kimeanza shughuli mbalimbali za kuelekea kilele cha maadhimisho hayo yatakayofanyika Mei 29 jumatatu wiki ijayo . Shughuli hizo ni za maendeleo Kwa ajili ya wananchi wa BERIBERATI mkoani Mambele kadei nchini humo CAR.

Uji wenye lishe bora kwa watoto walioathiriwa na kimbunga Freddy. Watoto walionufaika na mlo huu wako Mayela mjini Blantyre kusini mwa Malawi.
UNICEF/Thoko Chikondi

Watoto Malawi hatarini kukumbwa na utapiamlo, Umoja wa Mataifa wachukua hatua.

Takribani watoto 573,000 wenye umri wa chini ya miaka mitano nchini Malawi wako hatarini kukumbwa na utapiamlo, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto duniani,  UNICEF huku likisema linahitaji dola milioni 87.7 kukidhi mahitaji ya watu milioni 6.5 wakiwemo watoto milioni 3.3 nchini humo, ikiwa ni ombi jipya la fedha lililotolewa leo.

Sauti
2'13"