Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kiwanda cha uzalishaji wa nishati ya jua kata kisiwa cha Unguja nchini Tanzania.
World Bank

Benki ya Dunia yasaidia ukuzaji wa rasilimali watu na maendeleo nchini Tanzania

Tarehe 19 Desemba mwaka 2019, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio namba 74/245, ambalo liliteua tarehe 4 Desemba kuwa Siku ya Kimataifa ya Benki kwa kutambua mchango mkubwa wa benki za maendeleo za kimataifa na benki nyingine za maendeleo za kimataifa katika kuleta maendeleo endelevu na kuchangia uboreshaji wa hali za maisha za wananchi. 

Sauti
2'5"
Kikundi Cha Bendera cha Pamoja cha Walinda Amani wa Tanzani na Nepali wakitoa Salamu kwa Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani DRC, MONUSCO.
MONUSCO

Walinda amani wa MONUSCO kutoka nchini Tanzania na Nepal watunukiwa Nishani

Vikosi vya Walinda Amani kutoka Tanzania Kwa kushirikiana Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini Nepali wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemkorasia ya Kongo – DRC wamefanya gwaride la pamoja na kutunikiwa Nishani za Umoja wa Mataifa na Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani DRC, MONUSCO Luteni Jenerali Otavio Miranda Filho ikiwa ni kuthamini mchango wao wa kuhakikisha Amani ya Kudumu na Usalama vinapatikana nchini DRC.

Msichana mdogo nchini Zimbabwe anakunywa maji safi na salama kutoka kwenye kisima kilichorekebishwa kwa msaada wa Umoja wa Mataifa.
© UNICEF/Karin Schermbrucker

Ripoti: Mtoto 1 kati ya 3 anakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji - UNICEF

Mtoto mmoja kati ya Watoto watatu au sawa na watoto milioni 739 duniani kote - tayari wanaishi katika maeneo yaliyo na uhaba mkubwa au wa juu sana wa maji, na mabadiliko ya tabianchi yanatishia kufanya hali hii kuwa mbaya zaidi, imebainisha ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF iliyotolewa usiku wa kuamkia leo Jumatatu kwa saa za New York, Marekani.

Sauti
1'49"
(Maktaba) Mtoto akilia wakati mhudumu wa afya akimsogelea kutibu jeraha lake, Ni katika hospitali ya Al-Shifa mjini Gaza
UNICEF/Eyad El Baba

Maisha ya watoto yanaendelea kupotea Gaza huku hali ya kukata tamaa ikitawala: UN

Hali hatika hospitali za Gaza ni mbaya sana wagonjwa wakiendelea kupoteza maisha wakiwemo watoto njiti katika hospitali ya Al-Shifa ambayo kwa siku ya tatu mfululizo hakuna umeme huku mashambulizi ya Israel yakiongezeka, umesema Umoja wa Mataifa ambao leo unawaomboleza pia wafanyakazi wake 101 waliopoteza maisha katika mzozo huo na kusisitiza kwamba usitishwaji uhasama ni lazima sasa kuliko wakati mwingine wowote. 

Sauti
2'36"