Mashine 220 za kusaidia watoto wachanga kupata hewa ya oksijeni kutokana na kuwa hatarini kufariki dunia baada ya kuzaliwa ambazo zimetengenezwa nchini Kenya kwa msaada wa shirika la Umoja wa MAtaifa la kufanikisha upatikanaji wa dawa na tiba kwa gharama nafuu UNITAID zimepelekwa nchini Ukraine wakati huu ambapo vita vinakwamisha huduma za uzazi na kujifungua.
Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA, limetoa ombi la dola milioni 10.7 kwa ajili ya kutoa usaidizi wa kuokoa maisha kwa wanawake na wasichana zaidi ya milioni mbili nchini Sri Lanka.
Wiki ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa watoto ambayo ilianza tarehe mosi ya mwezi huu wa Agosti na kuadhimishwa duniani kote kwa jamii kuelimishwa kuhusu umuhimu wa mama kumnyonyesha mtoto imehitimishwa jana tarehe 7. Huko mkoani Morogoro nchini Tanzania, kwa wiki nzima mashirika mbalimbali kwa kushirikiana na serikali yamekuwa yakizungumza na wanajamii ili kufahamu uelewa wao kuhusu suala hili la unyonyeshaji na pia kuwapa elimu panapohitajika.
Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA, leo limetaja washindi 10 wa pamoja wa shindano la miradi bunifu inayoweza kuleta mabadiliko chanya na kuwezesha wanawake na wasichana duniani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO limesema umri wa kuishi barani Afrika tena akiwa na afya bora, umeongezeka kwa wastani wa miaka 10 kwa mtu mmoja kati ya mwaka 2000 na 2019, ikiwa ni ongezeko la kubwa kuliko ukanda mwingine wa shirika hilo duniani katika kipindi hicho hicho na sababu ni pamoja kuimarika kwa huduma za mama na mtoto.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, limesema nchi zinapaswa kushirikiana kukomesha haraka kuenea kwa ugonjwa wa ndui ya nyani, au Monkeypox bila kujali utaifa, rangi ya mtu au dini, amesema afisa mwandamizi wa shirika hilo hii leo.
Wakati zaidi ya robo tatu ya watu wazima wote wanaoishi na Virusi vya UKIMWI VVU wanapata aina fulani ya matibabu, idadi ya watoto wanaofanya hivyo, inafikia asilimia 52 pekee.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO leo limezindua ombi la takribani dola milioni 124 kwa ajili ya kushughulikia mahitaji ya haraka ya afya kwenye pembe ya Afrika hadi mwezi Desemba mwaka huu.
Wiki ya Unyonyeshaji watoto maziwa ya mama duniani imeanza rasmi hii leo chini ya kauli mbiu yake isemayo Kuongeza Unyonyeshaji: Elimisha na Usaidizi, Umoja wa Mataifa unatoa wito kwa serikali kutenga rasilimali zaidi ili kulinda, kukuza, na kusaidia sera na programu za unyonyeshaji, haswa kwa familia zilizo hatarini zaidi ambazo zinaishi katika mazingira ya dharura.
Zaidi ya Waafrika milioni 91 wanaishi na Ugonjwa wa Homa ya Ini aina B au C, ambayo ni aina mbaya zaidi ya virusi, kulingana na chapisho lililotolewa Julai 27,2022 kwenye wavuti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni WHO.