Perina Nakang alenga kushinda Olimpiki kuinua timu na familia yake
Perina Nakang, ni mmoja wa wanariadha 37 wanaounda timu thabiti ya wakimbizi kwenye michezo ya Olimpiki iliyoanza leo Julai 26 huko Paris, Ufaransa. Familia yake ilikimbia Sudan Kusini kwa sababu ya vita yeye akiwa na umri wa miaka 7 na kufika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya.