Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Tabianchi na mazingira

Ukumbi mkuu wa COP30 ambako kumefanyika ufunguzi wa mkutano huko   Belém, Brazil.
© UNFCCC/Kiara Worth

COP30 yataka ufadhili wenye usawa na kasi

Katika mkutano wa Nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi COP30 unaendelea huko mjini Belém, Brazil hoja moja imekuwa ikitawala: je, fedha za tabianchi zinaweza kugeuka kutoka ahadi kuwa msaada muhimu wa maisha kwa mataifa yaliyo kwenye mstari wa mbele wa athari za mabadiliko ya tabianchi?

Majanga ya asili husababisha mamilioni ya watu kuhama makazi yao kila mwaka.
IOM/Muse Mohammed

COP30 ni jukwaa kwa wakimbizi kupaza sauti juu ya athari za tabianchi kwao: Alfonso Herrera

Wiki ya kwanza ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP30, unaofanyika Belém Brazil, ikielekea ukingoni, viongozi wa dunia na wanaharakati wanakutana kujadili jinsi ya kushughulikia moja ya changamoto kubwa za wakati huu, ‘janga la mabadiliko ya tabianchi,” Na athari zake kwa wakimbizi hazikupewa kisogo. 

Sauti
2'57"
Mkutano kuhusu mabadiliko ya tabianchi unaanza Belém nchini Brazil Novemba 10, 2025
© UNFCCC/Diego Herculano

COP30: Watu waliofurushwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi watoa wito wa hatua za urekebishaji

Janga la tabianchi linaendelea kubadili ramani ya uhamaji wa watu duniani. Mafuriko, mawimbi ya joto, ukame na dhoruba vinalazimisha mamilioni ya watu kuzikimbia nyumba zao kila mwaka. Wengi wao hubaki ndani ya nchi zao, lakini bado wakikosa makazi salama. Wataalamu wanaonya kwamba katika miaka ijayo, mataifa mazima yanaweza kutoweka kutokana na kupanda kwa viwango vya bahari au ukame mkali unaozuia maisha.

Jamii nchini Jamaica zinasafisha mazingira baada ya uharibifu uliosababishwa na kimbunga Melissa.
© WFP/Arete

Maisha ni ngumu, uharibifu ni mkubwa baada ya kimbunga Melissa - Waathirika Jamaica

Wiki ya pili baada ya Kimbunga Melissa kupiga magharibi mwa Jamaica, mitaa ya Savanna-la-Mar na Watercress bado ipo kimya, kimya cha mji unaojaribu kujikwamua na Athari zilizoachwa na zahma hiyo. Nyumba zimebomoka, shule zimeharibiwa, maisha yamepinduliwa. Makadirio yanaonesha kuwa watu milioni 1.6 wameathirika, na sasa timu za misaada zinafanya kazi kwa haraka usiku na mchana kutoa msaada muhimu wa chakula, makazi, na usalama. 

UNDP inasaidia jamii za kampala nchini Uganda  kukabili mafuriko kwa kutengeneza mitaro.
© UNDP

Jinsi UNDP inavyosaidia jamii za kampala kukabili mafuriko

Kituo cha utafiti wa kusaka Suluhu kuhusu mafuriko kinachoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) nchini Uganda kimetumia maarifa ya pamoja kukabiliana na changamoto za mafuriko katika eneo la Makerere Kavule, makazi yasiyo rasmi yaliyo pembezoni mwa mji wa Kampala, mji mkuu wa Uganda. Kituo hicho kimeunganisha juhudi za jamii, maarifa asilia, na teknolojia ya kisasa kubuni mfumo wa mifereji ya maji unaoendana na Mpango Mkuu wa Mifereji ya Maji wa Jiji la Kampala (Kampala Capital City Drainage Master Plan). Mfumo huu unalenga kupunguza mafuriko si tu katika jamii hiyo, bali pia katika eneo la katikati ya jiji. 

Sauti
3'46"
Mifumo ya kupoeza ni mchangiaji mkubwa wa mabadiliko ya hali ya hewa.
© Unsplash/Sergei A

Mahitaji ya mifumo ya kupooza joto kuongezeka mara tatu ifikapo 2050: UNEP

Mahitaji ya mifumo ya baridi wa kupooza joto au viyoyozi yatarajiwa kuongezeka mara tatu ifikapo mwaka 2050, yakiendesha mabadiliko ya tabianchi na kuzidisha mzigo kwenye mifumo ya umeme kulingana na ripoti  ambayo imezinduliwa leo na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP Katika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP30 unaofanyika Belém, Brazili.