Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNGA78

MKUTANO WA 78 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Pata habari kutoka UNGA78

Jukwaa  limeandaliwa kwa ajili ya mjadala mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Wakati ulimwengu ukiendelea kukabiliwa na mdororo wa kijamii na kiuchumi kutokana na Covid 19 na athari zinazoendelea za vita nchini Ukraine, mjadala utafanyika kikamlifu ana kwa ana kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2019, na viongozi wa ulimwengu wakielekea NY kuwasilisha kauli zao katika Ukumbi mashuhuri. 

Hapa, Habari za UN inakupa kiti cha mstari wa mbele katika shughuli zote. Katika simu yako ya mkononi au kompyuta, fuatilia Wakuu wa Nchi na Serikali wanapofafanua hatua dhidi ya changamoto kubwa zaidi duniani na kushiriki katika majadiliano ya ngazi ya juu kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), hatua kabambe ya kumaliza janga la tabianchi, na vikao vitatu vya ngazi ya juu visivyo na kifani kuhusu afya: maandalizi dhidi ya majangahuduma ya afya kwa wote; na mapambano ya kimataifa dhidi ya kifua kikuu

Tutembelee kwenye majukwaa yetu ya mtandao wa kijamii

Twitter: twitter.com/HabarizaUN

Youtube: https://www.youtube.com/@UNNewsKiswahili 

Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu wakati akihutubia katika mjadala Mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
UN Photo/Laura Jarriel

Afrika ni ufunguo wa ulimwengu ujao - Rais Tinubu

“Afrika sio tatizo la kuepukwa na wala sio lakuonewa huruma. Afrika ni ufunguo wa ulimwengu ujao.” Ni kauli iliyotolewa na Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu wakati akihutubia katika mjadala Mkuu wa Mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa au UNGA78 jijini New York Marekani.

Phiona anafanya kazi katika kituo cha afya nchini Uganda kama mwanaharaki wa rika ya akina mama, anasaidia kutoa mafunzo na kusaidia akina mama kujifungua watoto wasio na VVU.
© UNICEF/Karin Schermbrucker

Viongozi wa dunia na wadau washikamana kutaka fursa sawa ya huduma za afya kwa wote: UNITAID

Wakati wa mkutano mkuu wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa wa mwaka huu, viongozi wa dunia, wadau wa afya na wawakilishi wa jamii wanaungana na shirika la kufanikisha upatikanaji wa dawa na tiba kwa gharama nafuu UNITAID, kutoa wito wa upatikanaji wa haraka na usawa zaidi wa bidhaa za afya zinazookoa maisha ili kuendeleza mchakato wa kupambana na changamoto kubwa zaidi za leo za afya, ikiwa ni pamoja na afya ya uzazi ya mama na mtoto, kuzuia majanga, kujiandaa na hatyua za kukabiliana na majanga, na virusi vya ukimwi VVU, kifua kikuu na malaria.

19 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Leo ni siku ya pili na ya mwisho wa mkutano kuhusu malengo ya maendeleo endelevu SDGs lakini leo pia ndio pazia la mjadala Mkuu wa 78, UNGA78 limefunguliwa na pamoja na na hotuba za viongozi pia kutakuwa na mikutano itakayo jadili hali za ulinzi na usalama katika mataifa mbalimbali na hapo kesho kutakuwa na mkutano wa ngazi ya juu kuhusu Sudan. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na nashinani ikimulika hotuba za viongozi katika Baraza Kuu na kazi za vijana katika utekelezaji wa DGs.  

Sauti
11'34"