Kiongozi wa kanisa katoliki duniani, Papa Francis amewasili nchini Iraq hii leo kwa ziara ya siku tatu, ziara ambayo shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO inasema ni ishara ya matumaini na fursa ya kuimarisha jitihada za amani, na umoja nchini humo.