Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Mtoto akipatiwa chanjo Gaza, kampeni inayoungwa mkono na WHO
© UNRWA/Ashraf Amra

Ukanda wa Gaza: Kampeni ya chanjo kwa watoto yazinduliwa

Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la kuhudumia watoto UNICEF, afya duniani WHO, linalohudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA na wizara ya afya ya Palestina wamezindua kampeni maalum ya chanjo, lishe na ufuatiliaji wa ukuaji wa watoto katika Ukanda wa Gaza, lengo likiwa ni kuwafikia watoto 44,000 waliokosa huduma muhimu za afya kutokana na vita vilivyodumu kwa miaka miwili.

Rais wa Baraza Kuu Annalena Baerbock (kushoto)akizungumza na kijana Ramadan aliyeandika simulizi kwa picha.
UN News/Abdelmonem Makki

Rais wa Baraza Kuu la UN awatembelea wakimbizi wa Kipalestina nchini Qatar

Rais wa mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Annalena Baerbock ametembelea wakimbizi wa kipalestina huko Doha nchini Qatar kuwajulia hali na kujionea maisha yao baada ya kuondolewa wakati wa vita kali huko Ukanda wa Gaza eneo la wapalestina linalokaliwa kimabavu na Israel na kuletwa nchini Qatar kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Leah Mushi anatupa taswira ya ziara yake hiyo.

Sauti
4'6"
Mvulana mdogo anahamishwa na timu za WHO kutoka Gaza
WHO screen capture

WHO yahamisha wagonjwa wa kwanza toka Gaza tangu usitishwaji mpya wa mapigano

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO, limeongoza uhamishwaji wa wagonjwa kutoka Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ikiwa ni  mara ya kwanza tangu kuanza kwa awamu mpya ya kusitishwa kwa mapigano kwenye  ukanda huo. Katika muda wa siku mbili, wagonjwa 41 waliokuwa katika hali mbaya pamoja na familia zao 145 wamehamishwa kutoka eneo la mgogoro, kuelekea Afrika Kusini, Uswisi na kwingineko, huku maelfu zaidi wakiendelea kusubiri matibabu ya dharura.

Sauti
3'24"
IOM inatoa mahema kote Gaza kwa familia zilizopoteza makazi ili kuwasaidia kukaa salama wakati msimu wa baridi unapokaribia.
© IOM

IOM yapeleka msaada wa makazi kwa Gaza kufuatia mahitaji makubwa baada ya kusitishwa kwa mapigano

Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limepeleka zaidi ya vifaa vya misaada 47,000 kwa Gaza tangu kutangazwa kwa usitishaji wa mapigano tarehe 10 Oktoba 2025 ili kusaidia familia zilizofurushwa. Kati ya vifaa hivyo, 31,000 ni vya makazi, ikiwa ni pamoja na mahema 2,500, ili kusaidia watu kujenga tena hisia za usalama na utu wao katikati ya uharibifu mkubwa. Imesema taarifa iliyotolewa leo hii huko Geneva/Amman.