Vichwa vya Habari
Makala Maalum
Malengo ya Maendeleo Endelevu
Kupunguza upotevu na utupaji wa chakula kuna jukumu muhimu katika kubadilisha mifumo ya kilimo na chakula. Kati ya malengo 17 ya Maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ambayo yanafikia kilele mwaka 2030 lengo namba 2 linahimiza kutokomeza njaa, lengo namba 8 linahimiza kazi nzuri na ukuaji wa kiuchumi na lengo namba 12 lina himiza utumiaji na uzalishaji wenye kuwajibika lengo likiwa kuwa na mifumo endelevu ya utumiaji wa rasilimali. Malengo yote haya yanaenda sambamba na harakati za kupunguza upotevu na utupaji wa chakula.
Habari kwa Picha
Umoja wa Mataifa: Kitovu cha diplomasia ya dunia
Viongozi kutoka kote ulimwenguni walirejea katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani katika mkutano wa kwanza kabisa wa ana kwa ana tangu janga la COVID-19 kuikumba duniani, na wameshiriki katika wiki ya kwanza ya mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa au UNGA78.
Habari Nyinginezo
Msaada wa Kibinadamu
Mwaka mmoja tangu mafuriko makubwa yakumbe Pakistan, bado usaidizi unasuasua na hii leo viongozi waandamizi wa Umoja wa Mataifa wamekutana kwenye kikao maalum na kutoa ahadi za usaidizi zaidi wakati taifa hilo la Asia likiendelea na mchakato mgumu wa kujijenga upya.
Amani na Usalama
Mratibu Maalum wa Umoja wa Mataifa wa Mchakato wa Amani ya Mashariki ya leo Jumatano ameelezea wasiwasi wake mkubwa kuhusu upanuzi usiokoma wa makazi ya walowezi wa Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikiwemo Jerusalem Mashariki.