UN News

Makala Maalum

Malengo ya Maendeleo Endelevu Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa maji wa 2023, ambao utafanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuanzia tarehe 22-24 Machi, unasifiwa kama fursa ya kipekee ya kizazi hiki ya kuharakisha maendeleo kuelekea upatikanaji wa maji salama na usafi wa mazingira ifikapo mwaka 2030.

Habari Nyinginezo

Tabianchi na mazingira Ripoti iliyotolewa na Jopo la Umoja wa Mataifa  linalohusika na masuala ya mabadiliko ya tabianchi (IPCC), inaelezea chaguzi nyingi ambazo zinaweza kuchukuliwa sasa, ili kupunguza uzalishaji wa gesi chafu na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi yanayosababishwa na binadamu.
Afya Wakati viongozi wa dunia wakijiandaa kuhudhuria mkutano wa kihistoria wa maji wa Umoja wa Mataifa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF llimetoa wito wa uwekezaji wa haraka katika huduma za maji, usafi na usafi wa mazingira (WASH) zilizo na mnepo ili kuwalinda watoto.