Vichwa vya Habari
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Masuala ya UM
Kwa nini ni muhimu:
Uteuzi wa Katibu Mkuu wa 10 wa Umoja wa Mataifa, atakayechukua madaraka kuanzia Januari 2027, unaweza kuathiri diplomasia ya kimataifa, mwitikio wa migogoro duniani, na mwelekeo wa mfumo wa ushirikiano wa kimataifa kwa muongo ujao.
Habari kwa Picha
Sudan: Safari ndefu ya uponyaji
Mgogoro wa kivita nchini Sudan ukikaribia kuingia mwaka wa 3, umezua janga kubwa zaidi la wakimbizi duniani kote kwa sasa, huku mamilioni ya raia wakilazimika kukimbia makazi yao kwenye maeneo ya kimkakati kama vile jimbo la Kordofan. Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, UNFPA linasema takribani watu milioni 13.6 wamepoteza makazi yao, ambapo milioni 9.3 wamesaka hifadhi ndani ya nchi na wengine milioni 4.3 wakivuka mipaka kutafuta hifadhi nchi jirani.
Habari Nyinginezo
Amani na Usalama
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, limeeleza wasiwasi mkubwa kufuatia kuuawa kwa wafanyakazi wawili waliokuwa wamepewa kandarasi na shirika hilo ya kusambaza maji safi kwa familia katika Ukanda wa Gaza.
Ukuaji wa Kiuchumi
Mawaziri wa kilimo kutoka kote barani Afrika wamekutana mjini Nouakchott, mji mkuu wa Mauritania, kujadili namna ya kuharakisha juhudi za kupunguza njaa kwa msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO).