Vichwa vya Habari
Makala Maalum
Malengo ya Maendeleo Endelevu
Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa maji wa 2023, ambao utafanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuanzia tarehe 22-24 Machi, unasifiwa kama fursa ya kipekee ya kizazi hiki ya kuharakisha maendeleo kuelekea upatikanaji wa maji salama na usafi wa mazingira ifikapo mwaka 2030.
Habari kwa Picha
UNICEF yawakinga na baridi kali baadhi ya wanavijiji wa Pakistani walioathiriwa na mafuriko
Miezi minne na nusu tangu kutangazwa kwa hali ya dharura kutokana na mafuriko makubwa yaliyokumba Pakistan kuanzia mwaka jana 2022, bado watu wako katika uhitaji mkubwa wa usaidizi kwa kuzingatia kuwa janga hilo la mafuriko limeambatana na msimu wa baridi. Miongoni mwa mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayotoa msaada ni lile la kuhudumia watoto UNICEF.
Habari Nyinginezo
Tabianchi na mazingira
Ripoti iliyotolewa na Jopo la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya mabadiliko ya tabianchi (IPCC), inaelezea chaguzi nyingi ambazo zinaweza kuchukuliwa sasa, ili kupunguza uzalishaji wa gesi chafu na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi yanayosababishwa na binadamu.
Afya
Wakati viongozi wa dunia wakijiandaa kuhudhuria mkutano wa kihistoria wa maji wa Umoja wa Mataifa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF llimetoa wito wa uwekezaji wa haraka katika huduma za maji, usafi na usafi wa mazingira (WASH) zilizo na mnepo ili kuwalinda watoto.