Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Wanawake
“Hakuna kitu kinachochangia mtu yeyote apigwe, auawe au kuchukuliwa mali” Ni Kauli ya Viola Jeptoo Lagat, Mwanariadha na Mchechemuzi wa masuala ya wanawake na wasichana kutoka Kenya, ambaye pia ni Mwanzilishi wa shirika lisilo la kiserikali la Tirop Angels liloloanzishwa wakati mwanariadha mwenzake Agnes Tirop kuuawa aliporejea nyumbani baada ya kuvunja rekodi za mashindano ya Olimpiki mwaka wa 2021 huko Ujerumani.
Habari kwa Picha
Mradi wa UNEP umesaidia wakulima Gambia kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ili kuzuia wimbi la vijana wanaoondoka nchini.
Mabadiliko ya tabianchi yamekuwa tishio kubwa kwa wakulima wadogo katika maeneo ya mashariki mwa Gambia, ambapo ukame, dhoruba kali na mmomonyoko wa ardhi vimeathiri uzalishaji wa chakula na kipato cha jamii. Kupitia mradi unaoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) kwa usaidizi wa Green Climate Fund, wakulima wamepata mafunzo na msaada wa kitaalamu unaowezesha uzalishaji endelevu na kuongeza ustahimilivu dhidi ya athari za tabianchi. Hadithi hii inaangazia safari yao ya mabadiliko kutoka changamoto hadi mafanikio wakijenga mustakabali bora kupitia kilimo kinachohimili mabadiliko ya hali ya hewa.
Habari Nyinginezo
Masuala ya UM
Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) kwa kushirikiana na Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Wanaojitolea (UNV) wamezindua mtandao mpya wa ulezi kwa ajili ya kuwasaidia wahamiaji wanaorejea katika nchi zao za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Amani na Usalama
Dharura inayoendelea kaskazini mwa Msumbiji inazidi kuwa mbaya, huku mashambulizi yanayoendelea kufanywa na makundi yenye silaha yasiyo ya kiserikali katika jimbo la Nampula yakisababisha ongezeko kubwa la wakimbizi wa ndani na kufanya kuwa moja ya mawimbi makubwa zaidi ya wakimbizi wa ndani mwaka huu, umeonya leo Umoja wa Mataifa.