Vichwa vya Habari
Makala Maalum
Wanawake
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC walinda amani aw Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye kikosi cha 5 cha utayari, TANZQRF-5 wameelezea ni kwa vipi wanasongesha ujumbe wa mwaka huu wa siku ya wanawake duniani, wa “Haki, Sheria, Hatua kwa wote Wanawake na Wasichana.”
Habari kwa Picha
Hakuna kurudi nyuma: Wanawake wanaendelea kutetea Haki na Sawa
Kwa karne nyingi, wanawake wamepambania haki sawa, fursa na uhuru. Kutoka kwa wanaharakati wa kupigania kura hadi wanaharakati wa kidijitali, kila kizazi kimevunja vizingiti na kusukuma mipaka. Dunia imepiga hatua, lakini maendeleo bado ni ya polepole, dhaifu na yasiyo sawa. Hakuna muda wa kurudi nyuma. Tunapoelekea 8 Machi – Siku ya Kimataifa ya Wanawake duniani, tunasonga mbele kwa ajili ya wanawake na wasichana wote.
Habari Nyinginezo
Wanawake
Kikao cha 70 cha Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani CSW70 kimefungu pazia hii leo jijini New York Marekani, mwaka huu kikibeba maudhui “Haki, haki ya kisheria na Hatua kwa wanawake na wasichana wote”. Zaidi ya washiriki 9000 wakiwemo wawakilishi wa serikali, asasi za kiraia, Umoja wa Mataifa na mashirika yake na wadau wengine wanatarajiwa kushiriki jukwaa hili litakalokunja jamvi 19 Machi likijumuisha mikutano ya kando 750.
Utamaduni na Elimu
Nilipopata taarifa kuwa ninarejea shuleni, nilihisi furaha mno, ndivyo asemavyo Sanita Wilson Lucas, mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 13 ambaye alilazimika kuacha masomo ya elimu ya msingi kwa sababu wazazi wake hawakumudu vifaa vya shule.