Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Malengo ya Maendeleo Endelevu
Kwa kuwa duniani kuna takriban wakimbizi milioni 42 na shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) zinafanyika katika maeneo mbalimbali duniani, (UNHCR) hukusanya na kutumia kiasi kikubwa cha data kutoka vyanzo mbalimbali.
Habari kwa Picha
Umoja wa Mataifa na juhudi za kupambana na Ebola huko DRC
Tangu kutangazwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola uliosababishwa na virusi aina ya Bundibugyo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC na Kampala nchini Uganda, mashirika ya Umoja wa Mataifa yakiongozwa na lile la Afya ulimwenguni WHO yamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kila hatua inachukuliwa katika kudhibiti mlipuko huo, kutibu waliopata maambukizi, kuelimisha jamii kujikinga na ugonjwa huo ili usizidi kuenea. Ndani ya wiki moja tangu kutangazwa kwa janga hilo la afya ya umma, WHO ilifanikiwa kusafirisha vifaa tiba kuingia DRC.
Habari Nyinginezo
Amani na Usalama
Nchini Sudan Kusini, Redio ndiyo chanzo kikuu cha taarifa kwa takribani asilimia 60 ya wananchi wa nchi hiyo changa zaidi barani Afrika. Ndiyo maana kuendelea kwa matangazo ya Radio Miraya ambayo yamedumu kwa miaka 20 katika redio hii inayomilikiwa na UNMISS yaani Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani Sudan Kusini ni kipaumbele cha juu katika juhudi zake za kuzuia migogoro na kujenga amani.
Amani na Usalama
Mashambulizi na mashambulizi ya kulipiza kisasi kati ya Iran na Marekani katika eneo la Ghuba yamezidisha hofu ya kurejea kwa vita kamili, huku Marekani ikikanusha madai ya Iran kwamba Jumapili ya Julai 12 ilikuwa imefunga Mlango Bahari wa Hormuz, njia muhimu ya kimataifa ya usafirishaji wa meli.