Vichwa vya Habari
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Masuala ya UM
Je, itachukua nini kwa Palestina kuwa Nchi Mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa? Wakati Baraza la Usalama linashughulikia suala hilo wakati vita vya uharibifu huko Gaza vikiingia mwezi wake wa saba, tuliangalia hali ya sasa ya Palestina na kile kinachohitajika kuwa Nchi Mwanachama wa Umoja wa Mataifa.
Habari kwa Picha
Sudan: Hadithi za maumivu na mateso katika mwaka wa vita
Soha na Suhaila Ahmed, mwenye umri wa miaka 12, ni mapacha kutoka jiji la Nyala huko Darfur. Vita nchini Sudan viliwalazimu kutoroka pamoja na mama yao na mdogo wao hadi mji wa Port Sudan ulioko mashariki ya mbali ya Sudan, katika safari ngumu ya mabasi na malori ya mizigo, iliyochukua umbali wa kilomita 2,360. Wasichana hao wawili, mama yao mgonjwa, na mdogo wao wa kiume walipata makazi ya muda katika bweni la wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Port Sudan, wakisubiri kurejea Khartoum baada ya vita kuisha. Wasichana hao wawili wanangojea hatima isiyojulikana. Nilishangazwa na nguvu na uvumilivu wa wasichana hawa wawili na kwamba bado waliweza kutabasamu na kuwa na matumaini baada ya kupitia uzoefu huo mgumu.
Habari Nyinginezo
Afya
Leo ni siku ya Malaria duniani ambapo mwaka huu inahamasisha kuongeza mapambano dhidi ya ugonjwa huu ili kuwa na ulimwengu wenye usawa zaidi kwani imebainika kuwa watu wanaoishi katika mazingira magumu ndio wanaoathirika zaidi.
Msaada wa Kibinadamu
Jumuiya ya kimataifa ina jukumu na wajibu wa kufanya kazi kufanikisha kukwamuka kwa Gaza lakini hatuwezi kuwaambia raia wasubiri, amesema afisa wa Umoja wa Mataifa anayehusika na ufikishaji wa misaada kwenye eneo hilo lililozingirwa na Israel.