Vichwa vya Habari
Habari Moto Moto
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Sheria na Kuzuia Uhalifu
Wakati dunia ikikabiliwa na ongezeko la uhalifu wa kupangwa, biashara haramu ya binadamu na matumizi ya dawa za kulevya, mwanamke kutoka Afrika Mashariki amepewa jukumu kubwa la kusaidia kuongoza mapambano ya kimataifa dhidi ya changamoto hizo.
Habari kwa Picha
Umoja wa Mataifa na juhudi za kupambana na Ebola huko DRC
Tangu kutangazwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola uliosababishwa na virusi aina ya Bundibugyo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC na Kampala nchini Uganda, mashirika ya Umoja wa Mataifa yakiongozwa na lile la Afya ulimwenguni WHO yamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kila hatua inachukuliwa katika kudhibiti mlipuko huo, kutibu waliopata maambukizi, kuelimisha jamii kujikinga na ugonjwa huo ili usizidi kuenea. Ndani ya wiki moja tangu kutangazwa kwa janga hilo la afya ya umma, WHO ilifanikiwa kusafirisha vifaa tiba kuingia DRC.
Habari Nyinginezo
Amani na Usalama
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amekaribisha tangazo kwamba Marekani na Iran zimefikia makubaliano ya amani yanayojumuisha usitishaji wa mapigano wa haraka na wa kudumu, kufunguliwa tena kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz pamoja na mfumo wa kuendeleza mazungumzo ya kisiasa.
Amani na Usalama
Mfululizo wa mashambulizi yaliyofanywa katika vitongoji vya kusini mwa mji wa Beirut siku wa kuamkia leo Jumapili umeonesha kwa mara nyingine hali tete ya mazungumzo ya amani yanayoendelea kuhusu Mashariki ya Kati imesema taarifa ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo na msemaji wake mjini New York Marekani.