Wanaotegemea msaada wa kibinadamu wana hali tete
Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la chakula na kilimo FAO na la mpango wa Chakula duniani WFP yameeleza jitihada za kupambana na kuongezeka kwa ukosefu wa usalama wa chakula zinazofanyika katika nchi kadhaa zinashindikana kutokana na kuwepo kwa mapigano na vizuizi ambavyo vimekwamisha ufikishaji misaada ya kuokoa maisha ya familia zinazokabiliwa na njaa.















