Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Wanawake
Kila mwaka ya Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hali ya Wanawake dunini (CSW) hukutana mwezi Machi kujadili namna ya kukabiliana na ukosefu wa usawa ulioenea, unyanyasaji na ubaguzi wa wanawake unaoendelea kuwakabili duniani kote.
Habari kwa Picha
Uwekezaji kwa wanawake ulivyoleta mabadiliko chanya kwenye jamii mashinani
Maudhui ya siku ya wanawake duniani mwaka huu wa 2024 ni Wekeza kwa Wanawake - Chochea Maendeleo. Maudhui haya tayari yamejidhihirisha wazi kuanzia Afrika, Asia, Mashariki ya Kati, Amerika hadi Ulaya kwani mashirika ya Umoja wa Mataifa yamebeba jukumu la kuchochea kasi ya kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kupitia wanawake. Habari Picha hii ni kithibitisho.
Habari Nyinginezo
Amani na Usalama
Hii leo huko jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kikosi cha 10 cha Tanzania (TANZBATT-10) kilichoko kwenye brigedi ya mapigano (FIB) ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO imekabidhi majukumu kwa kikosi cha 11, TANZBATT-11, katika hafla iliyofanyika eneo la Beni-Mavivi. Msimulizi wetu ni Kapteni Abubakari Muna, Afisa Habari wa TANZBATT-10.
Wanawake
Mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani, CSW68 ukiwa umeingia siku yake ya 5 leo, Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imekuwa ikizungumza na washiriki kutoka mataifa mbalimbali. Leo ni baadhi ya washiriki kutoka Tanzania, vinara wa elimu wanaofadhiliwa na Mfuko wa Malala.