Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus ameonya kile alichosema ni ukosefu wa usawa katika usambazaji na upatikanaji wa chanjo dhidi ya Corona au COVID-19 licha ya kwamba chanjo hiyo imepatikana katika kipindi kifupi zaidi kulinganishwa na chanjo zingine.