Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tuna imani Tanzania tutafikia lengo la huduma za afya kwa wote 2030: Waziri Ummy

Tuna imani Tanzania tutafikia lengo la huduma za afya kwa wote 2030: Waziri Ummy

Pakua

Tanzania taifa lililo Afrika Mashariki limesema limejipanga vyema katika kutekeleza azimio la kuchukua hatua kuhusu huduma za afya kwa wote lililoidhinishwa kwa kauli moja mwishoni mwa juma na nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa hapa Makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani. Waziri wa afya wa Tanzania Ummy Mwalimu alikuwa miongoni mwa waliohudhuria na ameketi chini na Flora Nducha wa Idhaa hii na kumfafanulia mikakati yao ya kutekeleza azimio hilo.

Audio Credit
Selina Jerobon/Flora Nducha
Audio Duration
5'52"
Photo Credit
UN News