Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kimataifa

Teknolojia ya droni nayo inaweza kuwa na manufaa bora au hasara kwa kutegemea inatumika kwenye misingi ipi. Hapa ni kwenye maonyesho ya ya mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu data uliofanyika Dubai 2018
IISD/ENB

Akili Mnemba (AI) ilete nuru na si giza – Katibu Mkuu UN

Hii leo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu amani na usalama duniani likimulika fursa na hatari zitokanazo na Akili Mnemba au Akili Bandia, AI ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesihi Baraza hilo lioneshe uongozi katika nyanja hiyo hasa katika kuhakikisha teknolojia hiyo inatumika kujenga madaraja ya kijamii, kidijitali na kiuchumi badala ya kuleta utengano na uharibifu.