Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP27

Mkutano wa UN wa Mabadiliko ya Tabianchi: COP27
6 Novemba - 18 Novemba 2022: Sharm el-Sheikh, Misri
...

Ikikabiliwa na ongezeko la janga la uhaba wa nishati, halikadhalika hewa chafuzi na matukio mabaya zaidi ya hali ya hewa, COP27 inasaka kurejesha tena mshikamano kati ya mataifa na kutekeleza Mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya wakazi wa dunia na sayari dunia.

Wakuu wa nchi, serikali, mawaziri, wasuluhishi pamoja na wanaharakati wa tabianchi, mameya, wawakilishi wa mashirika ya kiraia, watendaji wa kuu wa kampuni watakutana katika mji wa pwani ya Misri, Sharm el-Sheikh katika mkutano mkubwa kuhusu tabianchi.

Mkutano huo wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, UNFCCC, COP27 utasongesha yale yaliyokubaliwa kwenye CO26 na kutoa hatua zinazoendana na kutatua dharura ya tabianchi – kuanzia kupunguza hewa chafuzi, kutekeleza ahadi za kufadhili hatua kwa tabianchi katika nchi zinazoendelea.

21 NOVEMBA 2022

Hii leo jarida linaangazia siku ya uvuvi, masuala ya watoto na makala tunakwenda nchini Somalia kumulika uhakika wa chakula kwa watu waliokumbwa na changamoto ya ukame na mafuriko, mashinani ni ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Sauti
12'29"
COP27 yakamilisha kazi yake huko Sharm el-Sheikh, Misri kwa kufanya maamuzi makubwa.
Kiara Worth

COP27 yafikia tamati kwa kufanya maamuzi makubwa kuhusu ‘hasara na uharibifu’ 

Baada ya siku kadhaa za mazungumzo makali yaliyoendelea hadi Jumapili asubuhi kwa saa za Sharm el-Sheikh, Misri, nchi katika mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP27, zimefikia makubaliano kuhusu matokeo ambayo yalianzisha utaratibu wa ufadhili wa kufidia walioko katika hatari ya 'hasara na uharibifu' kutokana na majanga ya tabianchi yanayosababishwa na wanadamu.

Ina Maria Shikongo, mwanaharakati wa watu wa jamii ya asili kutoka Namibia akiwa kwenye maandamano huko COP27 Sharm-el-Sheikh nchini Misri.
UN News/Laura Quinones

Wanaharakati huko COP27 wasema hakuna hatua kwa tabianchi bila kujali haki za binadamu

Huko Sharm-el-Sheikh nchini Misri, kwenye mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP27, tarehe 17 mwezi huu wa Novemba yalishuhudiwa maandamano ya maelfu ya wawakilishi wa watu wa jamii ya asili, wanawake, wanarahakati wa masuala ya jinsia, vijana, mazingira na haki kwa tabianchi kutoka pande mbalimbali za dunia.

Sauti
3'51"
Laura Quinones

Wanaharakati huko COP27 wasema hakuna hatua kwa tabianchi bila kujali haki za binadamu

Huko Sharm-el-Sheikh nchini Misri, kwenye mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP27, tarehe 17 mwezi huu wa Novemba yalishuhudiwa maandamano ya maelfu ya wawakilishi wa watu wa jamii ya asili, wanawake, wanarahakati wa masuala ya jinsia, vijana, mazingira na haki kwa tabianchi kutoka pande mbalimbali za dunia. Wao waliandamana kwa niaba ya maelfu ya mashirika na mamilioni ya watu  na kupitisho azimio lao la umma kuhusu haki kwa tabianchi. Wanapaza sauti je ni sauti zipi? Wanataka nini? Anold Kayanda amefuatilia maandamano hayo na kuandaa Makala haya..

Sauti
3'51"
Skrini ya jumla ya COP27 inaonyesha logan rasmi ya Urais wa Misri: "Pamoja kwa Utekelezaji".
UNIC Tokyo/Momoko Sato

COP27 ikielekea ukingoni Guterres atawaka washiriki kusimama kidete na kutimiza ahadi

Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP27 umepangwa kufunga pazia katika muda wa saa 24 zijazo, lakini nchi zimesalia kugawanyika katika masuala kadhaa muhimu ikiwa ni pamoja na hasara na uharibifu unaosababishwa na zahma hiyo ya kimataifa,  amesema leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na kuzitaka pande zote kuchukua hatua za haraka na kutimiza ahadi dhidi ya changamoto kubwa zaidi inayowakabili wanadamu. 

17 NOVEMBA 2022

Hii leo jaridani tunaangazia mada kwa kina na leo tunafunga safari hadi bara Hindi huko nchini India kusikia kuhusu kijiji cha kwanza nchini humo kinachotumia nishati ya sola pekee kwa wakazi wake zaidi ya 6,400.  Pia litakuletea Habari kwa ufupi kama zifuatayo:

Sauti
12'23"
DRC
© FAO/Thomas Nicolon

Kulinda bayoanuwai inamaanisha kulinda mkataba wa mabadiliko ya tabianchi wa Paris: COP27

Wakati kwa miaka mingi mzozo wa hmabadiliko ya tabianchi na mzozo wa bioanuwai umechukuliwa kama maswala tofauti, ukweli kama ulivyoangaziwa katika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi wa COP27 leo ni kwamba hakuna njia ya kuhakikisha kiwango cha joto duniani kinasalia nyuzi joto 1.5 ° C bila kuchukua hatua haraka kulinda maliasili. 

16 Novemba 2022

Hii leo jaridani tunaangazia mabadiliko ya tabianchi na athari kwa wakimbizi, ziara ya afisa wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan, Makala tunamulika haki za wenye ualbino Uganda na mashinani tunamulika nafasi ya wananawake kwenye maamuzi.

Sauti
13'28"

15 NOVEMBA 2022

Leo katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa tunakuletea Habari kwa Ufupi zikimulika idadi ya watu kufikia bilioni 8, Mada kwa Kina tunakupeleka Peru kumulika wanawake wa jamii ya asili na upandaji miti, na Mashinani tunamulika polisi wa Umoja wa Mataifa na ulinzi wa amani.

1. Habari Kwa Ufupi:

Sauti
12'12"