Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP27

Mkutano wa UN wa Mabadiliko ya Tabianchi: COP27
6 Novemba - 18 Novemba 2022: Sharm el-Sheikh, Misri
...

Ikikabiliwa na ongezeko la janga la uhaba wa nishati, halikadhalika hewa chafuzi na matukio mabaya zaidi ya hali ya hewa, COP27 inasaka kurejesha tena mshikamano kati ya mataifa na kutekeleza Mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya wakazi wa dunia na sayari dunia.

Wakuu wa nchi, serikali, mawaziri, wasuluhishi pamoja na wanaharakati wa tabianchi, mameya, wawakilishi wa mashirika ya kiraia, watendaji wa kuu wa kampuni watakutana katika mji wa pwani ya Misri, Sharm el-Sheikh katika mkutano mkubwa kuhusu tabianchi.

Mkutano huo wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, UNFCCC, COP27 utasongesha yale yaliyokubaliwa kwenye CO26 na kutoa hatua zinazoendana na kutatua dharura ya tabianchi – kuanzia kupunguza hewa chafuzi, kutekeleza ahadi za kufadhili hatua kwa tabianchi katika nchi zinazoendelea.

Mtoto akiwa amesimama karibu na pampu ya maji iliyozingirwa na maji ya mafuriko huko Gatumba nchini Burundi.
© UNICEF/Karel Prinsloo

Haki za binadamu ni moyo wa juhudi za kukabiliana athari za tabianchi: Türk

Kuelekea mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa Tabianchi, COP27 huko Sharm el-Sheikh nchini Misri, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu Volker Türk amesema anatarajia matokeo ya mkutano huyo yatazingatia haki ya kila mtu ya kuishi ambaypo kwa sasa ipo hatarini kutokana na uwepo wa hatua zisizotosheleza za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Mtoto mwenye umri wa miaka 11 akijipatia ahueni ya joto kali kwa kucheza kwenye chemchem ya maji huko  Uzbekhstan
UNICEF/Pirozzi

Watoto milioni 559 duniani kote wanataabika na joto kali kwa sasa, idadi itaongeza na kufikia zaidi ya bilioni 2 mwaka 2050.

Kuelekea mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP27utakaofanyika nchini Misri barani Afrika, shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto UNICEF wametoa ripoti ya kuonesha athari za mabadiliko ya tabianchi kwa watoto katika kipindi cha kuanzia sasa mpaka mwaka 2050.

Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Tabianchi.
UN /Cia Pak

Madhara ya tabianchi yanachanja mbuga, hatua kwa tabianchi zinadorora- UN

Wawakilishi wa serikali wakianza kukamilisha ajenda kwa ajili ya mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP27 utakaofanyika mwezi ujao huko Misri, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewaambia waandishi wa habari jijini New York, Marekani kuwa kazi iliyo mbele ni kubwa na nzito wakati huu ambapo madhara ya tabianchi yanashuhudia kote duniani.