Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP27

Mkutano wa UN wa Mabadiliko ya Tabianchi: COP27
6 Novemba - 18 Novemba 2022: Sharm el-Sheikh, Misri
...

Ikikabiliwa na ongezeko la janga la uhaba wa nishati, halikadhalika hewa chafuzi na matukio mabaya zaidi ya hali ya hewa, COP27 inasaka kurejesha tena mshikamano kati ya mataifa na kutekeleza Mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya wakazi wa dunia na sayari dunia.

Wakuu wa nchi, serikali, mawaziri, wasuluhishi pamoja na wanaharakati wa tabianchi, mameya, wawakilishi wa mashirika ya kiraia, watendaji wa kuu wa kampuni watakutana katika mji wa pwani ya Misri, Sharm el-Sheikh katika mkutano mkubwa kuhusu tabianchi.

Mkutano huo wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, UNFCCC, COP27 utasongesha yale yaliyokubaliwa kwenye CO26 na kutoa hatua zinazoendana na kutatua dharura ya tabianchi – kuanzia kupunguza hewa chafuzi, kutekeleza ahadi za kufadhili hatua kwa tabianchi katika nchi zinazoendelea.

Benki ya Dunia/Bamidele Emmanuel Oladokun

Mabadiliko ya tabianchi yaweka njiapanda vijana Afrika kuhusu suala la kupata watoto

Takriban nusu ya vijana barani Afrika wamesema wanafikiria upya suala la kupata watoto ama la kutokana na mabadiliko ya tabianchi, kwa mujibu wa ripoti mpya ya matokeo ya kura ya maoni iliyoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF bakwa kuwahoji watu 243,512 duniani kote. Taarifa ya Flora Nducha inafafnua zaidi  

Sauti
2'55"

09 NOVEMBA 2022

Karibu katika jarida la Habari za UN hii leo ambalo kwa kiasi kikubwa linamulika harakati za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na wakati huo huo hatua za kuchukua wakati huu ambapo mabadiliko ya tabianchi yanaathiri jamii mbalimbali duniani.

Sauti
13'13"