Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP27

Mkutano wa UN wa Mabadiliko ya Tabianchi: COP27
6 Novemba - 18 Novemba 2022: Sharm el-Sheikh, Misri
...

Ikikabiliwa na ongezeko la janga la uhaba wa nishati, halikadhalika hewa chafuzi na matukio mabaya zaidi ya hali ya hewa, COP27 inasaka kurejesha tena mshikamano kati ya mataifa na kutekeleza Mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya wakazi wa dunia na sayari dunia.

Wakuu wa nchi, serikali, mawaziri, wasuluhishi pamoja na wanaharakati wa tabianchi, mameya, wawakilishi wa mashirika ya kiraia, watendaji wa kuu wa kampuni watakutana katika mji wa pwani ya Misri, Sharm el-Sheikh katika mkutano mkubwa kuhusu tabianchi.

Mkutano huo wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, UNFCCC, COP27 utasongesha yale yaliyokubaliwa kwenye CO26 na kutoa hatua zinazoendana na kutatua dharura ya tabianchi – kuanzia kupunguza hewa chafuzi, kutekeleza ahadi za kufadhili hatua kwa tabianchi katika nchi zinazoendelea.

Skrini ya jumla ya COP27 inaonyesha logan rasmi ya Urais wa Misri: "Pamoja kwa Utekelezaji".
UNIC Tokyo/Momoko Sato

COP27 ikielekea ukingoni Guterres atawaka washiriki kusimama kidete na kutimiza ahadi

Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP27 umepangwa kufunga pazia katika muda wa saa 24 zijazo, lakini nchi zimesalia kugawanyika katika masuala kadhaa muhimu ikiwa ni pamoja na hasara na uharibifu unaosababishwa na zahma hiyo ya kimataifa,  amesema leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na kuzitaka pande zote kuchukua hatua za haraka na kutimiza ahadi dhidi ya changamoto kubwa zaidi inayowakabili wanadamu. 

17 NOVEMBA 2022

Hii leo jaridani tunaangazia mada kwa kina na leo tunafunga safari hadi bara Hindi huko nchini India kusikia kuhusu kijiji cha kwanza nchini humo kinachotumia nishati ya sola pekee kwa wakazi wake zaidi ya 6,400.  Pia litakuletea Habari kwa ufupi kama zifuatayo:

Sauti
12'23"