Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP27

Mkutano wa UN wa Mabadiliko ya Tabianchi: COP27
6 Novemba - 18 Novemba 2022: Sharm el-Sheikh, Misri
...

Ikikabiliwa na ongezeko la janga la uhaba wa nishati, halikadhalika hewa chafuzi na matukio mabaya zaidi ya hali ya hewa, COP27 inasaka kurejesha tena mshikamano kati ya mataifa na kutekeleza Mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya wakazi wa dunia na sayari dunia.

Wakuu wa nchi, serikali, mawaziri, wasuluhishi pamoja na wanaharakati wa tabianchi, mameya, wawakilishi wa mashirika ya kiraia, watendaji wa kuu wa kampuni watakutana katika mji wa pwani ya Misri, Sharm el-Sheikh katika mkutano mkubwa kuhusu tabianchi.

Mkutano huo wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, UNFCCC, COP27 utasongesha yale yaliyokubaliwa kwenye CO26 na kutoa hatua zinazoendana na kutatua dharura ya tabianchi – kuanzia kupunguza hewa chafuzi, kutekeleza ahadi za kufadhili hatua kwa tabianchi katika nchi zinazoendelea.

DRC
© FAO/Thomas Nicolon

Kulinda bayoanuwai inamaanisha kulinda mkataba wa mabadiliko ya tabianchi wa Paris: COP27

Wakati kwa miaka mingi mzozo wa hmabadiliko ya tabianchi na mzozo wa bioanuwai umechukuliwa kama maswala tofauti, ukweli kama ulivyoangaziwa katika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi wa COP27 leo ni kwamba hakuna njia ya kuhakikisha kiwango cha joto duniani kinasalia nyuzi joto 1.5 ° C bila kuchukua hatua haraka kulinda maliasili. 

16 Novemba 2022

Hii leo jaridani tunaangazia mabadiliko ya tabianchi na athari kwa wakimbizi, ziara ya afisa wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan, Makala tunamulika haki za wenye ualbino Uganda na mashinani tunamulika nafasi ya wananawake kwenye maamuzi.

Sauti
13'28"