Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP27

Mkutano wa UN wa Mabadiliko ya Tabianchi: COP27
6 Novemba - 18 Novemba 2022: Sharm el-Sheikh, Misri
...

Ikikabiliwa na ongezeko la janga la uhaba wa nishati, halikadhalika hewa chafuzi na matukio mabaya zaidi ya hali ya hewa, COP27 inasaka kurejesha tena mshikamano kati ya mataifa na kutekeleza Mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya wakazi wa dunia na sayari dunia.

Wakuu wa nchi, serikali, mawaziri, wasuluhishi pamoja na wanaharakati wa tabianchi, mameya, wawakilishi wa mashirika ya kiraia, watendaji wa kuu wa kampuni watakutana katika mji wa pwani ya Misri, Sharm el-Sheikh katika mkutano mkubwa kuhusu tabianchi.

Mkutano huo wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, UNFCCC, COP27 utasongesha yale yaliyokubaliwa kwenye CO26 na kutoa hatua zinazoendana na kutatua dharura ya tabianchi – kuanzia kupunguza hewa chafuzi, kutekeleza ahadi za kufadhili hatua kwa tabianchi katika nchi zinazoendelea.

Mitambo ya sola katika ofisi za UNDP jijini Dar es Salaam nchini Tanzania kama sehemu ya kuongoza kwa vitendo katika hatua za kulinda mazingira.
Sawiche Wamunza/UNDP Tanzania

Tanzania kushirikiana na SADC kuzalisha nishati jadidifu

Wakati wiki ya kwanza ya mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP27 unaondelea huko Sharm el-Sheikh nchini Misri ikiwa inaelekea ukingoni na masuala mbalimbali yakiwa yamejadiliwa ikiwemo ufadhili wa miradi ya tabianchi, malipo ya fidia kwa nchi maskini kutokana na hasara na uharibifu uliosababishwa na madhara ya mabadiliko ya tabianchi, Tanzania imeitisha mkutano na nchi wanachama Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika, SADC ili kuhimiza ushirikiano katika kuzalisha nishati jadidifu.

10 NOVEMBA 2022

Katika Jarida la habari la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea 

-Huko Sharm el Sheikh kwenye mkutno wa COP27 vijana watoa wito kwa nchi wachafuzi wa mazingira kugharamia hasara na uharibifu wa janga hilo

-Nchini Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo DRC ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO washikana na jeshi la serikali FARDC kuendesha doria kulinda raia

-Nchini Lebanon shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na wadau wa chanjo wafikisha chanjo 600,000 kwa ajili ya kampeni dhidi ya kipindupindu itakayoanza Jumamosi

Sauti
13'40"
Benki ya Dunia/Bamidele Emmanuel Oladokun

Mabadiliko ya tabianchi yaweka njiapanda vijana Afrika kuhusu suala la kupata watoto

Takriban nusu ya vijana barani Afrika wamesema wanafikiria upya suala la kupata watoto ama la kutokana na mabadiliko ya tabianchi, kwa mujibu wa ripoti mpya ya matokeo ya kura ya maoni iliyoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF bakwa kuwahoji watu 243,512 duniani kote. Taarifa ya Flora Nducha inafafnua zaidi  

Sauti
2'55"

09 NOVEMBA 2022

Karibu katika jarida la Habari za UN hii leo ambalo kwa kiasi kikubwa linamulika harakati za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na wakati huo huo hatua za kuchukua wakati huu ambapo mabadiliko ya tabianchi yanaathiri jamii mbalimbali duniani.

Sauti
13'13"
Sayari badala ya Faida! Ndio kauli mbiu inayotumiwa na waandamanaji wakiwa wanataka viongozi waweke sayari mbele badala ya faida.
© Unsplash/Markus Spiske

Ahadi hewa na ulaghai wa kampuni kuhusu hatua kwa tabianchi vikome – Katibu Mkuu UN

Ingawa serikali nyingi na kampuni zinatoa ahadi za kudhibiti utoaji wa hewa chafuzi sambamba na mikakati ya kufyonza ile inayozalishwa, vigezo vya kuzingatia ahadi hizo vina upenyo mkubwa na mpana wa kuwezesha ahadi hizo kutotekelezwa, amelalama hii leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wakati huu ambapo jopo maalum alilounda kuhusu tabianchi likichapisha ripoti iliyofuatilia ahadi hewa za kudhibiti utoaji hewa chafuzi. 

Green Care nchini Rwanda imekuja na suluhisho endelevu la kukusanya taka nchini humo.
UN/Flora Nducha

Tuliona fursa katika kuchakata taka na hatukusita tukaichangamkia: Greencare Rwanda

Taka zinazotupwa hivyo bila utaratibu maalum wa kuzidhibiti  ni mtihani mkubwa kwa jamii nyingo hususan barani Afrika na kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa athari zake ni mbaya kiafa na kimazingira. Lakini vijana katika wilaya ya Huye iliyoko jimbo la Kusini mwa Rwanda hawakuona athari tuu za kiafya au mazingira katika kudhibiti taka hizo bali waliona fursa pia hasa za ajira na kiuchumi, ndipo walipoamua kulivalia njuga sula hilo na kuanzisha mradi wa Green care  

08 NOVEMBA 2022

Hii leo katika Habari za UN tunakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Mashinani na zote zikiwa ne mrengo wa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi unaofanyika huko Sharm el-Sheikh nchini Misri.

Sauti
10'38"