Umoja wa Wapalestina unahitaji kuleta amani:Ban
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kuwa shughuli za kuleta mapatano miongoni mwa wapalestina lazima zifanyike kwa njia ambayo itachangia kuwepo kwa amani na usalama.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kuwa shughuli za kuleta mapatano miongoni mwa wapalestina lazima zifanyike kwa njia ambayo itachangia kuwepo kwa amani na usalama.
Afisa wa ngazi ya juu katika masuala ya mabadiliko ya hali ya hewa kwenye Umoja wa Mataifa amesema kuwa ufadhili mpya utakaozisadia nchi zinazoendelea kukabiliina na mabadiliko ya hali ya hewa unahitaji kuwatia moyo wawekezaji wa kibinafsi.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa katika kuchagiza na kulinda haki ya uhuru wa maoni na kujieleza Frank La Rue amesema serikali lazima zichangie na kuleta mabadiliko badala ya kukandamiza watu.
Ufaransa ambayo itakuwa ni rais wa mzunguko kwenye baraza la usalama mwezi huu wa Mai inasema itajikita katika maeneo yanayoghubikwa na machafuko mwezi huu.
Mwakilishi maalumu wa vikosi vya pamoja vya Umoja wa Mataifa na muungano wa Afrika kulinda amani Darfur UNAMID Ibrahim Gambari amezindua mradi maalumu wenye lengo la kuongeza fursa kwa mashirika ya msaada wa kibinadamu ili kuwafikia maelfu ya watu katika jamii zilizoathirika na vita na ambazo ni vigumu kufikika kwenye jimbo la Darfur.
Ripoti mpya iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD kuhusu uwekezaji wa moja kwa moja wa nje (FDI) katika nchi 48 masikini kabisa duniani, imetaka kuwe na mabadiliko ya mtazamo ili kusaidia kutoa nafasi za ajira pamoja na kuinua hali ya maisha katika nchi hizo, kuziwezesha kuzalisha bidhaa nyingi na zilizo tofauti.
Watu takribani wanane wameuawa nchini Uganda na wengine wengi kujeruhiwa wakati majeshi ya usalama yalipowakabili waandamanaji waliokuwa wakipinga kupanda kwa gharama za maisha.
Kifo cha kiongozi wa Al Qaeida Osama Bin Laden pia kimetoa afueni kwa maelfu ya watu kwenye nchi za Afrika ya Mashariki hususani Kenya na Tanzania ambako mamia ya watu waliuawa katika shambulio la kwanza la kigaidi eneo hilo mwaka 1998.
Mwanzilishi na kiongozi wa mtandao wa kigaidi wa kimataifa wa Al Qaeda , bwana Osama Bin Laden ameuawa na majeshi ya Marekani nchini Pakistan.
Kampeni ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa kutanabaisha umuhimu wa chanjo katika kuokoa maisha hususani ya watoto itamalizika Jumapili wiki hii baada ya wiki nzima iliyoambatana na chanjo, mafunzo, maonesho na mijadala duniani kote.