Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UNAMID imetangaza mipango ya kibinadamu kusaidia Darfur

Mwakilishi maalumu wa vikosi vya pamoja vya Umoja wa Mataifa na muungano wa Afrika kulinda amani Darfur UNAMID Ibrahim Gambari amezindua mradi maalumu wenye lengo la kuongeza fursa kwa mashirika ya msaada wa kibinadamu ili kuwafikia maelfu ya watu katika jamii zilizoathirika na vita na ambazo ni vigumu kufikika kwenye jimbo la Darfur.

Uwekezaji usaidie ajira na hali ya maisha:UNCTAD

Ripoti mpya iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la biashara na maendeleo UNCTAD kuhusu uwekezaji wa moja kwa moja wa nje (FDI) katika nchi 48 masikini kabisa duniani, imetaka kuwe na mabadiliko ya mtazamo ili kusaidia kutoa nafasi za ajira pamoja na kuinua hali ya maisha katika nchi hizo, kuziwezesha kuzalisha bidhaa nyingi na zilizo tofauti.