Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Amani itapatikana Afrika Magharibi kwa kuwapokonya silaha wapiganaji

Baraza la usalma la Umoja wa Mataifa wiki hii limesema upokonaji silaha na kuwarudisha katika maisha ya kawaida wapiganaji wa zamani na kukomesha tatizo kubwa la biashara haramu ya silaha ndogo ndogo ni hatua muhimu kabisa ambazo nchi za Afrika ya Magharibi zinabidi kuchukua ikiwa amani itadumishwa katika eneo hilo.

Wakuu wa UM wanataka Wa-Kongo wasubiri matokeo rasmi

Likiwapongeza wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa kushiriki katika uchaguzi wa kihistoria wa nchi yao, kwa sehemu kubwa kabisa kwa amani, siku ya Jumapili, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilitoa mwito wiki hii kuwataka wawe watulivu na kusubiri matokeo ya mwisho ya uchaguzi.

Jaribio la Mapinduzi lagunduliwa Burundi

Afisi ya kulinda amani ya UM huko Burundi ONUB imeeleza kushangazwa na ripoti kua kulikuwepo na jaribio la kuipindua serekali ya Bujumbura, siku chache zilizopita na kwamba kuna wanasiasa mashuhuri walotiwa vizuizini.

UNICEF kulaani vitendo vya ubakaji wa watoto Zimbabwe

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto UNICEF limelaani vikali sana habari za kutokea vitendo zaidi vya ubakaji huko Zimbabwe na likihimiza sheria mpya kupitishwa kuwalinda watoto wa nchi hiyo na kutoa masomo zaidi juu ya virusi vua HIV na Ukimwi.