Walinda amani watatu wa MINUSCA kutoka Tanzania wamejeruhiwa nchini CAR
Walinda amani watatu wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzaina wanaohudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR ujulikanao kama MINUSCA wamejeruhiwa jana Alhamisi katika kijiji cha Batouri Bole, mkoani Mambéré-Kadéï baada ya gari lao kukanyaga kilipuzi.