Lebanon: Haki imetendeka, Mahakama Maalum yafunga pazia, Guterres atuma shukrani
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amepongeza kazi kubwa na ngumu iliyofanywa na majaji na wafanyakazi wa Mahakama Maalum kwa ajili ya Lebanon, iliyoanzishwa kuwajibisha wahusika wa shambulio la Februari 14 mwaka 2005 huko Beirut. Mahakama hiyo imemaliza muda wake leo Jumapili Desemba 31, baada ya kufanya kazi kwa miaka 14.