Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hukumu ikisomwa wakati wa kesi dhidi ya Ayyash na wenzake baada ya kupatiakana na hatia ya mauaji kwenye shambulio la mwaka 2005 huko Beirut, Lebanon. (Maktaba)
Mahakama Maalum kwa Lebanon

Lebanon: Haki imetendeka, Mahakama Maalum yafunga pazia, Guterres atuma shukrani

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amepongeza kazi kubwa na ngumu iliyofanywa na majaji na wafanyakazi wa Mahakama Maalum kwa ajili ya Lebanon, iliyoanzishwa kuwajibisha wahusika wa shambulio la Februari 14 mwaka 2005 huko Beirut. Mahakama hiyo imemaliza muda wake leo Jumapili Desemba 31, baada ya kufanya kazi kwa miaka 14.

Mtoto akiwa katika kambi ya wakimizi wa ndanijimboni Ituri nchini DRC  kufuatia kufurushwa makwao kutkana na mapigano mashariki mwa nchi
© UNICEF/Diana Zeyneb Alhindawi

Kikosi cha kwanza cha SADC chawasili DRC kusaidia kukabili mapigano mashariki mwa nchi

Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wanajeshi wa kikosi cha kwanza kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika, SADC kitakachokuwa na jukumu la kusaidiana na jeshi la serikali, FARDC kujibu mashambulizi kutoka kwa vikundi vilivyojihami mashariki mwa nchi hiyo, wamewasili huko Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.

Audio Duration
1'37"
Moja ya familia iliyotawanywa kutoka Al Ganoub Oktoba 2023.
OCHA/Manal Massalha

Watoto waliouawa Ukingo wa Magharibi na Jerusalem Mashariki, idadi haijawahi kushuhudiwa

Mwaka huu umekuwa mwaka mbaya zaidi kuwahi kurekodiwa kwa watoto katika Ukingo wa Magharibi, ikiwa ni pamoja na Jerusalem Mashariki, huku ghasia zinazohusiana na migogoro zikifikia kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa, amesema Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF kanda ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Adele Khodr.