Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashariki ya Kati

Mashariki ya Kati

Ahmed Fayyad alikuwa mwanafunzi wa ufamasia sasa anauza mboga huko a majaniDeir Al-Balah  baada ya mapigano kumfurusha huko Khan Younis, Ukanda wa Gaza.
UN News / Ziad Taleb

Katika zama hizi za mvutano, tulivyo kwenye hatari ya kutumbukia kwenye korongo huko Mashariki ya Kati, ni wajibu wangu kama Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa natoa maombi makuu mawili. Kwa Hamas, mateka wote waachiliwe huru haraka bila masharti. Kwa Israeli, fungua njia haraka bila vikwazo ili misaada ya kibinadamu na wahudumu wa kiutu kwa ajili ya raia Gaza.

Katibu Mkuu wa UN katika taarifa yake kuhusu Mashariki ya Kati 15 Oktoba 2023

MAELEZO

Umoja wa Mataifa unashirikiana na wadau wa kikanda na kimataifa katika juhudi zake za kuondoa mvutano, huku ukihamasisha kuimarika kwa hali bora kwenye eneo hilo, na kusongesha mashauriano ya kisiasa ili hatimaye kutimia kwa jawabu la kuweko kwa mataifa mawili yaani Israeli na Palestina pamoja na amani ya kina, ya kudumu Mashariki ya Kati.

UN NA SUALA LA PALESTINA

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (katikati) akijibu maswali kutoka kwa vyombo vya habari kwenye kivuko cha Rafah.

Katibu Mkuu

Katibu Mkuu huchukua hatua yeye mwenyewe binafsi au kupitia wajumbe wake kwa maslahi ya diplomasia ya kuzuia mizozo, kusaka amani na ujenzi wa amani Mashariki ya Kati. Halikadhalika yeye huwakilisha Umoja wa Mataifa kwenye mazungumzo ya pande nne kuhusu Mashariki ya Kati, Quartet. Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwenye Mchakato wa Amani Mashariki ya Kati humwakilishi Katibu Mkuu kwenye masuala yote yanayohusu mchakato wa amani.

Baraza Kuu

Taswira ndani ya ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wakati Katibu Mkuu António Guterres alipohutubia ufunguzi wa Mjadala Mkuu wa UNGA77

Baraza Kuu la UN , linaloundwa na wajumbe wote wanachama wa Umoja wa Mataifa, limekuwa likijihusisha na katika kusaka suluhu ya amani kwenye Suala la Palestina tangu mwaka 1947. Kamati ya kusimamia Haki zisizopingika za Watu wa Palestina ilianzishwa na Baraza Kuu mwaka 1975.

Baraza la Usalama

Baraza la Usalama lina wajibu wa msingi wa kulinda amani na usalama duniani. Baraza limeshughulikia suala la Mashariki ya Kati na Suala la Palestina katika matukio kadhaa.

UNRWA

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, (UNRWA) kwa kiasi kikubwa ndio lenye operesheni kubwa zaidi za Umoja wa Mataifa huko Mashariki ya Kati, likitoa huduma za afya, elimu, misaada na huduma za kijamii kwa zaidi ya wakimbizi milioni 5 wa kipalestina walioko Jordan, Lebanon, Syria, Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan ikiwemo Yerusalemu Mashariki.

UNTSO

Hili ni shirika la Umoja wa Mataifa la kusimamia Mikataba, (UNTSO) liliidhinishwa na Baraza la Usalama huko Palestina mwaka 1948, operesheni ya kwanza ya ulinzi wa amani kuanzishwa na Umoja wa Mataifa.

Baraza la Haki za binadamu

Baraza la Umoja wa Mataifa la  Haki za Binadamu  limeshughulikia suala la Palestina wakati wa vikao vyake vya kawaida na maalum. Hufanya kazi kwa karibu na Mtaalamu Maalum kuhusu hali ya haki za binadamu kwenye maeneo ya Palestina yanayokaliwa tangu 1967.

UNSCO

UNSCO ni ofisi inayomwakilishi Katibu Mkuu na huongoza mfumo wa Umoja wa Mataifa kwnye juhudi zote za kisiasa na kidiplomasia zinazohusiana na  mchakato wa amani ikiwemo Mazungumzo ya pande nne (Quartet). UNSCO pia huratibu kazi za kiutu na maendeleo za mashirika ya Umoja wa Mataifa na program kwenye maeneo ya Palestina yanayokaliwa na Israeli, kwa kusaidia mamlaka za Palestina na wapalestina.