Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kampeni ya chanjo ya surua inayolenga watoto milioni 14 ilizinduliwa nchini Ethiopia. (Maktaba)
© UNICEF/Nahom Tesfaye

Ethiopia yaanza kampeni ya kitaifa ya chanjo ya surua inayolenga zaidi ya watoto milioni 15.5

Taarifa iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, imeeleza kuwa Wizara ya Afya ya Serikali ya Shirikisho (MoH) la Ethiopia imezindua rasmi kampeni jumuishi ya chanjo ya surua nchini kote tangu tarehe 22 Desemba 2022 katika hafla iliyosimamiwa na Waziri wa Afya wa Jimbo Dkt Dereje Duguma katika Kituo cha Afya cha Siriti katika Mji Mdogo wa Akaki Kaliti huko Addis Ababa.

© UNICEF/Delil Souleiman
Mtoto akiwa kwenye kambi ya muda huko Ain Issa nchini Syria. (3 Juni 2019)

Theluthi moja ya watu kwenye nchi za Kiarabu wanaishi katika umasikini: ESCWA

Kwa mujibu wa utafiti mpya uliotolewa leo na tume ya Umoja wa Mataifa ya kiuchumi na kijamii kwa mataifa ya Asia Magharibi ESCAWA kuhusu maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwenye ukanda wa nchi za Kiarabu asilimia kubwa ya watu katika ukanda huo wanaishi chini ya mstari wa umasikini licha ya ukuaji wa uchumi. 

Muuguzi akiwa amesimama katika wodi ya watoto wachanga katika hospitali moja mjini Gardez, Afghanistan
© UNICEF/Mihalis Gripiotis

Ushiriki wa wanawake katika utoaji na ufikishaji wa misaada Afghanistan lazima uendelee: UN na wadau

Uamuzi wa mamlaka ya Afghanistan wa kuwapiga marufuku wanawake kufanya kazi katika mashirika ya kibinadamu yasiyo ya kiserikali NGO’s umeendelea kulaaniwa na wadau mbalimbali kutoka jumuiya ya kimataifa yakiwemo mashirika ya Umoja wa Mataifa wakisema ni pigo kubwa kwa jamii zilizo hatarini, kwa wanawake, kwa watoto, na kwa nchi nzima kulingana.