Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Gari ambalo limeharibiwa  na Tsunami katika kijiji cha  Labuhan, Pandeglang, Banten, Indonesia.
UNICEF/Arimacs Wilander

Matukio ya mwaka 2018 .

Leo Jumatatu ya tarehe 31 mwezi Desemba mwaka 2018, mwisho wa mwaka  jarida la Habari za Umoja wa Mataifa limemulika matukio muhimu ya mwaka huu wa 2018. Hata hivyo tumekuwekea pia habari zilizogongwa vichwa hii leo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Yemen na Afghanistan.

Mtoto huyu pichani mwenye umri wa miezi miwili ni mkazi wa Hajjah, nchini Yemen na ana unyafuzi. Mzozo unaoendelea nchini Yemen unasababisha mamilioni ya watu wawe hatarini kukumbwa na baa la njaa.
WFP/Marco Frattini

Chakula cha msaada Yemen chauzwa sokoni- WFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakuka WFP linataka kukomeshwa mara moja kwa hatua ya kupelekwa kwingine msaada wa chakula nchini Yemen baada ya kugundua mchezo mchafu unaofanywa katika mji mkuu wa Sana’a  na sehemu zingine zinazosimamiwa na kundi la Houthi wa kupeleka chakula maeneo yasiyokuwa yamelengwa na msaada huo.

Baadhi ya nyumba za  mtaa wa Shejaiya Gaza zilizoharibiwa na mlipuko wa bomu na ikiwa haina maji wala umeme.
UNICEF/El Baba

Huku misaada ikipungua, mwaka wa 2018 umeshudia ongezeko la majeruhi kwa wapelestina: OCHA

Kwa mujibu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada OCHA, kwa mwaka huu wa 2018, vikosi vya Israel vimewauwa wapalestina 295 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 29,000, hii ikiwa ndiyo idadi kubwa ya vifo kuwahi kutokea kwa mwaka mmoja tangu mgogoro wa Gaza uanze mwaka 2014 na pia kuwa na idadi kubwa ya majeruhi tangu tangu OCHA ianze fuatilia majeruhi katika eneo la Palestina linalokaliwa, maarufu kama oPt.

Maandalizi ya uchaguzi huko DRC
MONUSCO/Alain Likota

Kila mmoja ana jukumu la kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani-Guterres

Wakati wananchi wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC wakihesabu saa kuelekea uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na majimbo unaotarajiwa kufanyika jumapili hii desemba 30, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika taarifa yake aliyoitoa kupitia msemaji wake hii leo mjini New York Marekani, amewasihi mamlaka nchini DR Congo, viongozi wa kisiasa wa pande zote, tume ya uchaguzi CENI na jumuiya za kijamii kuendelea kushirikiana ili kuhakikisha kunakuwa na mazingira yasiyo na vurugu kusudi siku ya uchaguzi wapiga kura wote wanaostahili waweze kupiga kura zao kwa amani.

Viongozi wa wanawake DRC wakiwakilisha  sekta zote za asasi za kiraia, wakiwa na Leila Zerrougui, Mkuu wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, MONUSCO
MONUSCO/John Bompengo

Inasikitisha baadhi ya raia wa DRC hawatashiriki uchaguzi huu muhimu-Bi Zerrougui

Leila Zerrougui, Mwakilishi Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, amesema kuwa anasikitika kwamba kuna raia ambao hawataweza kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaofanyika jumapili hii ya tarehe 30 mwezi huu wa Desemba nchini humo, kufuatia uamuzi wa Tume Huru ya Taifaya uchaguzi ya nchi hiyo, CENI, kuahirisha upigwaji kura katika maeneo ya Beni, Butembo na Yumbi kwa sababu ya mlipuko wa Ebola na ukosefu wa usalama.