Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mapigano nchini Libya yamezidhisha adha kwa raia

Shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR linasema kuwa mapigano yanayoendelea katika eneo la Dehiba kwenye mpaka kati ya Libya na Tunisia yamewazuia wakimbizi wanaokimbia kutoka magharibi mwa Libya likisema kuwa huenda wakimbizi hao wamejipata kati kati mwa mapigano kati ya serikali na wanaoipinga serikali.

Mashirika yasaidie kupambana na ufisadi:UNODC

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na madawa ya kulevya na uhalifu UNODC ametoa wito kwa sekta za umma na za kibinafsi kwenye nchi zilizostawi duniani kuchukua hatua ambazo zinaweza kuangamiza ufisadi akisema kuwa suala hilo linaweza kuzua mizozo.

CERF imesaidia mamilioni ya watu mwaka 2010:UM

Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia masuala ya kibinadamu kwa kuhakikisha msaada wa haraka kwa watu walioathirika na vita na majanga ya asili CERF, mwaka jana ulitenga dola milioni 415 ili kuyawezesha mashirika ya misaada kuwasaidia watu milioni 22 katika nchi 45.