Mapigano nchini Libya yamezidhisha adha kwa raia
Shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR linasema kuwa mapigano yanayoendelea katika eneo la Dehiba kwenye mpaka kati ya Libya na Tunisia yamewazuia wakimbizi wanaokimbia kutoka magharibi mwa Libya likisema kuwa huenda wakimbizi hao wamejipata kati kati mwa mapigano kati ya serikali na wanaoipinga serikali.