Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na Pale

Ofisi ya Msemaji wa KM imeripoti kwamba Ban Ki-moon anaendelea kushauriana, kwa kutumia njia ya simu, na maofisa wa UM wa vyeo vya juu waliokuwepo kwenye eneo la uhasama Mashariki ya Kati. Katika saa 24 zilizopita KM aliwasiliana na mawaziri wa nchi za kigeni wa Israel na Marekani, na KM anatazamiwa kuongeza juhudi zake katika siku zijazo katika kuhakikisha mwito wa kusimamisha mapigano katika eneo liliokaliwa la WaFalastina katika Tarafa ya Ghaza utahishimiwa.

Baraza la Usalama lakutana tena kusailia mgogoro wa Ghaza

Baraza la Usalama limekutana Ijumatano magharibi, kwenye kikao cha dharura, kuzingatia mswada wa azimio liliodhaminiwa na Libya, kwa niaba ya Mataifa Wanachama wa Umoja wa Nchi Huru za KiArabu, kuhusu uwezekano wa kusimamisha mapigano yaliozuka katika eneo la WaFalastina liliokaliwa la Tarafa ya Ghaza. Kwenye risala mbele ya kikao hicho, KM Ban Ki-moon alikumbusha ya kuwa mtiririko wa mgogoro uliofumka Ghaza siku ya leo umeingia siku ya tano. Alisema raia wa KiFalastina, wanaojumuisha mfumo wa jamii hakika ya Tarafa ya Ghaza, pamoja na mpango wa amani kwa siku za

Mkuu wa UNRWA asema hali, kijumla, ni 'mbaya sana' kwa sasa Ghaza

Kwenye mahojiano na Idara ya Habari ya UM Ijumanne, Karen AbuZayd, Kamishna Mkuu wa Shirika la UM la Kufarajia Wahamiaji wa KiFalastina wa Mashariki ya Karibu (UNRWA) alieleza ya kuwa hali ya vurugu katika Tarafa ya Ghaza hivi sasa, ni mbaya sana kushinda mifumko ya uhasama wa miaka iliopita, kwenye eneo hilo:~

Vikosi vya AMISOM Usomali vyapongezwa na KM kwa ujasiri wao

KM Ban Ki-moon amerudia tena mwito alioutoa hapo kabla, unaoyahimiza Mataifa Wanachama kuharakisha kuchangisha misaada ya fedha, pamoja na ile misaada inayohitajika kushughulikia usafirishaji wa watu na vitu, au lojistiki, ili kuhudumia bora operesheni za vikosi vya Umoja wa Afrika katika Usomali, yaani vikosi vya AMISOM.