Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewateua wanawake 20 katika nyadhifa za juu katika mwaka 2020
UN

Mwaka 2020 UN imeteua wanawake viongozi 20 na 2021 utafuata nyayo

Mwaka 2020 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameteua wanawake 20 kushikilia nyadhifa za juu za uongozi.

Wanawake tisa kati ya hao waliteuliwa katika nafasi za kisiasa au mipango ya amani mashinani. Na kati ya wanawake hao 9 wanatoka Afrika, 7 bara amerika na visiwa vya Caribbea, 3 bara Ulaya na 1 kutoka Asia. Basi leo tunawamulika wanawake hao 9 kutoka bara la Afrika ambao usikose kuwafuatilia mwaka 2021.

 

Shule ya Oumoul Mouminina katika eneo la  Forobaranga Darfur Magharibi ikilindwa na UNAMID
UNAMID/Albert González Farran

Asante UNAMID kazi mmeitimiza:UN/AU

Mwenyekiti wa tume ya muungano wa Afrika AU, Moussa Faki Mahamat na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres wakizungumzia maamuzi yaliyofanywa na Baraza la Muungano wa Afrika la amani na usalama na Baraza la Usalama la umoja wa Mataifa, leo ndio siku ya mwisho ya mpango wa pamoja wa vyombo hivyo viwili wa kulinda amani Darfur Sudan ujulikanao kama UNAMID.

Majaribio yanaonesha kwamba chanjo dhidi ya virusi vya corona ina uwezo mkubwa wa kuzuia hatariza COVID-19.
University of Oxford/John Cairns

WHO yataka ufuatiliaji na tahadhari Afrika wakati aina mpya ya COVID-19 imeibuka

Wakati hivi karibuni kumeibuka aina mpya ya virusi vya corona au COVID-19 barani Afrika ambavyo kiwango cha maambukizi yake ni cha juu zaidi, shirika la afya duniani WHO leo limetoa wito kwa nchi zote za bara hilo kuongeza kiwango cha ufuatiliaji na tathimini kupitia mtandao wa maabara Afrika ili kubaini mwenendo wowote mpya wa maambukizi na kuimarisha juhudi za kukabiliana na mlipuko huo.

Mtoto mwenye umri wa miezi saba, huko Yemen, akipimwa mzingo wa mkono ili  kuangalia utapiamlo. Mzozo unaoendelea umesababisha ukosefu mkubwa wa chakula kote nchini, na kuacha maelfu ya watoto wakiwa na utapiamlo uliokithiri..
UNICEF/Motaz Fuad

Mwaka 2021 watoto takribani milioni 10.4 watakabiliwa na utapiamlo uliokithiri-UNICEF  

Wakati mwaka 2021 unakaribia, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, lina wasiwasi kuhusu afya na ustawi wa watoto milioni 10.4 wanaokadiriwa kuugua utapiamlo uliokithiri mwaka ujao katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, kaskazini mashariki mwa Nigeria, Sahel ya Kati, Sudan Kusini na Yemen. Hizi ni nchi au kanda ambazo zinakabiliwa na majanga mabaya ya kibinadamu wakati pia zikikabiliwa na ongezeko la ukosefu wa chakula, janga hatari la corona.