Mwaka 2020 UN imeteua wanawake viongozi 20 na 2021 utafuata nyayo
Mwaka 2020 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameteua wanawake 20 kushikilia nyadhifa za juu za uongozi.
Wanawake tisa kati ya hao waliteuliwa katika nafasi za kisiasa au mipango ya amani mashinani. Na kati ya wanawake hao 9 wanatoka Afrika, 7 bara amerika na visiwa vya Caribbea, 3 bara Ulaya na 1 kutoka Asia. Basi leo tunawamulika wanawake hao 9 kutoka bara la Afrika ambao usikose kuwafuatilia mwaka 2021.