Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mkutano wa utunzaji misitu kufanyika Brazzaville:UM

Maafisa kutoka zaidi ya nchi 35 zilizo kwenye maeneo yaliyo na misitu mikubwa zaidi duniani wanatarajiwa kukusanyika kwenye mkutano unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa mwezi ujao kujadili changamoto zinazoyakumba maeneo hayo yaliyo tegemeo kwa zaidi ya watu bilioni moja.

UNIMIS yakaribisha maridhiano ya kumaliza mzozo Abyei

Ujumbe maalumu wa umoja wa mataifa nchini Sudan (UNMIS) amekaribisha hatua zilizochukuliwa za kufikiwa makubaliano ya pamoja kwa pande mbili zinazozana katika jimbo la Abyei ambazo zimeafiki kuunda kamati ya kufuatilia utekelezaji wa maridhiano yanayoyaka vikundi vya waasi kuachana na mienendo korofi.

UN-HABITAT yazindua jumuiya ya mtandao kusaidia miji

Shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT limezindua jumuiya mpya ya mtandao iitwayo URBAN GATEWAY ili kusaidia miji na wataalamu wa mipango miji duniani kuungana, kubadilishana uzoefu na kuchukua hatua kwa ajili ya kuwa na miji endelevu katika wakati huu ambapo miji inapanuka kwa kasi duniani.