Mkutano wa utunzaji misitu kufanyika Brazzaville:UM
Maafisa kutoka zaidi ya nchi 35 zilizo kwenye maeneo yaliyo na misitu mikubwa zaidi duniani wanatarajiwa kukusanyika kwenye mkutano unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa mwezi ujao kujadili changamoto zinazoyakumba maeneo hayo yaliyo tegemeo kwa zaidi ya watu bilioni moja.