Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mapitio ya Kazi za UM 2007

Mnamo mwaka 2007 UM ulikabiliwa na matatizo kadha wa kadha yaliohitajia suluhu ya pamoja, kutoka jamii ya kimataifa, kwa UM kufanikiwa kulinda usalama na amani na kuimarisha maendeleo ya uchumi na jamii yatakayokuwa na natija kwa umma pote duniani.

Hapa na pale

Kikundi Kazi cha Baraza Kuu kinachosimamia juhudi za kukomesha na kufyeka ukandamizaji wa kijinsia, na unyayanyasaji miongoni mwa watumishi wa UM, wamepitisha azimio muhimu karibuni litakalowahakikishia waathiriwa wa unyanyasaji wa kijinsia kuwa wanapatiwa tiba maridhawa, ushauri, misaada ya jamii na vile vile msaada wa kisheria.

Watoto wanadai haki zao

Hivi majuzi, Baraza Kuu la UM lilifanyisha kikao makhsusi cha siku tatu, kilichokuwa na lengo la kufuatilia utekelezaji wa nchi wanachama wa zile ahadi zilizopendekezwa mwaka 2002 kwenye mkutano mkuu wa UM, ambapo kulipitishwa ‘mpango wa utendaji’ wa kujenga mazingira salama yatakayotunza haki na maisha bora kwa watoto wote, pote ulimwenguni. Mpango huo ulipewa muktadha usemao “Ulimwengu Unaostahili Kuishi Watoto kwa Utulivu na Amani.”

Watumishi wa UM kuwakumbuka wenziwao waliouawa Algiers

Mapema wiki hii, mnamo tarehe 17 Disemba, watumishi wa UM walijumuika kote duniani kuwakumbuka wenziwao 17 waliouawa na shambulio la magaidi liliotukia Disemba 11 kwenye ofisi za UM mjini Algiers, Algeria. Wafanyakazi wa UM walikaa kimya kwa dakika moja kuheshimu kumbukumbu za wenziwao waliofariki Algiers.