Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Francine na watoto wake watatu walilazimika kuondoka kijijini kwake kutokana na mzozo usiokoma mashariki mwa DRC. Sasa wanapokea msaada wa WFP katika kambi ya wakimbizi wa ndani huko Kivu Kaskazini.
© WFP/Michael Castofas

WFP DRC waomba msaada wa $Mil 425 kusaidia wakimbizi wa ndani

Wakati Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemorkasia Kongo DRC ikiripoti kuwa na zaidi ya wakimbizi wa ndani 738,000 kwa kipindi cha mwaka huu wa 2024 pekee kutokana na kuongezeka kwa machafuko, Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limeeleza kuwa na uhitaji wa haraka wa dola milioni 425 ili waweze kuwasaidia wakimbizi hao wanaoongezeka kila uchao. 

Sauti
1'49"
Mitambo ya kuzalisha umeme kwa njia ya upepo kwenye barabara kuu ya pwani huko Yancheng, Uchina
© Yan Wang

Ushirikiano wa kimataifa utasaidia kuhamia haraka katika nishati jadidifu - Francesco La Camera

Ushirikiano wa kimataifa ni moja ya njia muhimu kuyafanya mataifa duniani  kuhamia  kwa haraka katika nishati mbadala na jadidifu. Na hiyo ni miongoni mwa juhudi zinazofanywa na Shirika la Kimataifa la Nishati Mbadala IRENA, kama anavyoeleza Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Francesco La Camera katika mahojiano na Jing Zhang wa Idhaa ya Kichina ya Umoja wa Mataifa.

Sauti
2'27"
Washiriki katika jukwaa na vijana la ECCOSOC Vivian Joseph (Kushoto) Mtatibu na mwakilishi wa kitengo chaafya kwa vijana wa SADC na Joramu Nkumbi (Kulia) mwenyekiti mtendaji wa jukwaa la viongozi vijana wa Afrika kwa upande wa Tanzania wakizungumza na Fl…
UN News

Vijana wa Afrika lazima tuchangamkie fursa na kujifunza toka kwa wenzetu: Joram Nkumbi na Vivian Joseph

Jukwaa la vijana la Baraza la kiuchumi na kijamii ECOSOC limekunja jamvi jana jioni hapa makaomakuu ya Umoja wa Mataifa ambapo zaidi ya vijana 1000 kutoka nchi zaidi ya 80 wameshiriki wakiwemo Vivian Joseph Afisa tabibu akiwasilisha vijana katika jumuiya ya maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika SADC na Joramu Nkumbi mkurugenzi mtendaji wa jukwaa la Afrika la viongozi vijana kwa upande wa Tanzania. 

Sauti
3'19"
UNICEF inafanya kazi na serikali ya Nigeria kuhakikisha kila mtoto anapata mazingira salama ya kujifunzia.
© UNICEF/Dawali David

Miaka 10 ya watoto kutekwa Chibok, bado hakuna mifumo ya ulinzi - UNICEF

Nigeria inapotimiza miaka 10 tangu tukio la utekwaji nyara la watoto wa kike 275 huko Chibok, kaskazini magharibi mwa taifa hilo, hadi sasa bado watoto 90 wamesalia mateka na nchi hiyo inasalia na kumbukumbu ya tukio linguine la wanafunzi wa shule kutekwa nyara jimboni Kaduna mwezi Machi mwaka huu, hali inayosababisha Umoja wa Mataifa kutoa wito mahsusi.

Sauti
2'58"