Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

SYRIA

Syria

Familia ya wakimbizi. mama na watoto wake katika kambi ya Al Hol nchini Syria.
UNICEF

“Wakimbizi kwenye kambi ya Al Hol kila mara wako hatarini kujeruhiwa au kuuawa. Zaidi ya matukio 90 ya mauaji na majaribio 40 ya mauaji yametokea Al Hol mwaka 2021 pekee. Tunarejelea wito wetu kwa nchi wanachama kuchukua wanawake na watoto kutoka kwenye kambi hiyo.”

Lynn Welchman, Kamishna, Tume Huru ya Kimataifa ya uchunguzi Syria

SYRIA

Tangu machi 2011, Syria imekuwa katika mgogoro ambao umewalazimisha watu zaidi ya 500,000 kutoroka makazi yao. Mamilioni ya raia wa Syria sio tu ni wamekimbia nchi yao, bali pia mamilioni wengine wamekuwa wakimbizi wa ndani. Mgogoro huu unachukuliwa kuwa mbaya zaidi wa kibinadamu kipindi hiki ambapo watu zaidi ya milioni 13 wanahitaji msaada na unalaumiwa kwa kusababisha wanaume, watoto pamoja na wanawake wengi wa Syria kutaabika.

 

HATUA ZA KIBINADAMU

Watu mamia kwa maelfu wameuawa na mamilioni wamelazimishwa kukimbia tangu Machi 2011, wakati mapigano yalipoanza nchini Syria kati ya serikali na makundi yanayotaka kumuondoa madarakani rais Bashar al- Assad. UN ikiwa na washirika wake inajaribu kutoa mahitaji ya msaada wa kibinadamu.

HABARI ZA UN KUHUSU SYRIA

Bofya hapa kupata habari za Umoja wa Mataifa kuhusu Syria.

 

MJUMBE MAALUM KUHUSU SYRIA

Mwezi Januari mwaka 2019, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alimteua Geir O. Pedersen kuwa mjumbe wake maalum wa 4 kwa Syria. Hivi sasa anaongoza jitihada za UN za kusongesha utekelezaji wa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa namba 2254 la mwaka 2015  na pia tamko la pamoja la Geneva la mwaka 2012. Bwana Pedersen anafanya kila juhudi kuweza kuleta kwenye meza ya mazungumzo , makundi yote yanayohusika ili kuweza kumaliza vita. mazungumzo yanazingatia azimio hilo namba 2254 yakimulika  utawala, ratiba na mchakato wa kupanga katiba mpya na kufanyika uchaguzi mkuu kama msingi wa mchakato wa Syria wa kumaliza mgogoro huo. Pia mazungumzo yanahusu mikakati dhidi ya ugaidi.