Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Ushelisheli yaongeza idadi ya wanachama wa mahakama ya ICC

Visiwa vya Ushelisheli vilivyo katika bahari ya Hindi vimekuwa nchi ya hivi karibuni kuwa mwanachama wa makahama ya kimakataifa kuhusu uhalifu ICC ambayo imepewa jukumu la kuwashtaki na kuwahukumu watu wanaokabiliwa na vitendo vya mauaji ya halaiki ,uhalifu wa kivita pamoja na uhalifu dhidi ya ubinadamu.

UM wataka taarifa kutoka kwa Hizbollah kuhusu mauaji ya Hariri

Mwendesha mashitaka katika mahakama inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa , iliyoundwa ili kuwahukumu washukiwa wa mauaji ya waziri mkuu wa zamani wa Lebanon Rafiq Hariri na wengine 22 imwitaka serikali kukabidhi taarifa zote zinazodaiwa kuhifadhiwa na kiongozi wa Hisbollah Hassan Nasrallah ambazo ni muhimu kwa ajili ya tukio hilo la 2005.