Ushelisheli yaongeza idadi ya wanachama wa mahakama ya ICC
Visiwa vya Ushelisheli vilivyo katika bahari ya Hindi vimekuwa nchi ya hivi karibuni kuwa mwanachama wa makahama ya kimakataifa kuhusu uhalifu ICC ambayo imepewa jukumu la kuwashtaki na kuwahukumu watu wanaokabiliwa na vitendo vya mauaji ya halaiki ,uhalifu wa kivita pamoja na uhalifu dhidi ya ubinadamu.