IOM yasaidia wahamiaji kupata taarifa Japan
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM linasaidia juhudi zinazoendelea za kusambaza taarifa kuhusu tetemeko na misaada ya dharura kwa jamii za wahamiaji zinazoeishi nchini Japan.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM linasaidia juhudi zinazoendelea za kusambaza taarifa kuhusu tetemeko na misaada ya dharura kwa jamii za wahamiaji zinazoeishi nchini Japan.
Mionzi ya nyuklia imeanza kusambaa moja kwa moja hewani kufuatia mlipuko katika mitambo ya nyuklia ya Japan iliyoharibiwa na tetemeko na tsunami limesema shirika la kimataifa la nguvu za atomic IAEA.
Tani 47 za msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF umewasili kwenye mji wa Ben Guerdane karibu na mpaka wa Tunisia na Libya.
Mapigano yakiongezeka nchini Libya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linahofu kwamba watu wanaotaka kukimbia vita na kutafuta hifadhi hawawezi kuondoka au wanazuiwa kuondoka.
Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Libya Abdel Elah Al-Khatib ameitaka serikali ya Libya kuruhusu bila pingamizi mashirika ya Umoja wa Mataifa ili yaweze kusaidia mamilioni ya Walibya na kuwapa msaada wanaouhitaji.
Haki za binadamu nchini Sudan zinaendelea kukiukwa na viongozi wa nchi hiyo amesema mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu Sudan.
Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP leo limeanza kuweka msingi wa kituo chake kipya cha masuala ya kifundi nchini Djibouti ambacho kitatumika kama kiungo cha shirika hilo kwenye pembe ya Afrika.
Mkurugenzi wa shilika la kazi duniani ILO leo amekaribisha tamko lililotolewa na wa kazi wa Misri kwamba jumuiya za wafanyakazi zitaorodhoshwa na kuruhusiwa kufanya kazi kwa uhuru na ameahidi msaada wa ILO katika kuboresha hali na mazingira ya kazi nchi humo.
Umoja wa Mataifa na mashirika yake mbalimbali umekuwa ukiendelea kutoa mchango mkubwa duniani katika njanja nyingi zikiwemo za kiuchumi, kijamii, kisiasa na kitamaduni.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki moon amesema kuwa kushikilia zaidi tamaduni na kutokuwepo uvumilivu huenda kukaongeza mwanya uliopo kati ya tamaduni mbali mbali duniani.