Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Jitokezeni kupiga kura yasema MINUSTAH Haiti

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Haiti umesema kuwa kuwepo kwa utulivu wa kisiasa na kukua kwa uchumi wa nchi hiyo kunategemea kwa upande mwingine idadi kubwa ya watu watakaojitokeza kupiga kura wakati wa duru ya pili ya uchaguzi wa urais unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki.

Misitu ni muhimu kutatua tatizo la maji:FAO

Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO leo limeonya kwamba ifikapo mwaka 2025 watu bilioni 1.8 watakuwa wakiishi kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa wa maji na theluthi mbili ya watu wote duniani watakabiliwa na matatizo ya maji .

Mkuu wa haki za binadamu amelaani mauaji ya raia Ivory Coast

Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay ameelezea hofu juu ya kuendelea kuzorota kwa hali ya usalama nchini Ivory Coast. Amesema mashambulizi dhidi ya raia hayakubaliki na kulaani mauaji ya jana kwenye kitongoji cha Abobo mjini Abidjan ambako makombora yamekatili maisha ya watu takriban 30 na kujeruhi wengine wengi.