Vikosi ya UNOCI vyashambuliwa Ivory Coast
Askari kadhaa wa umoja wa mataifa wa kulinda amani nchini Ivory Coast wameshambuliwa na kujeruhiwa.
Askari kadhaa wa umoja wa mataifa wa kulinda amani nchini Ivory Coast wameshambuliwa na kujeruhiwa.
Watu wa Libya wanahitaji msaada wa kimataifa wakati wakijaribu kupata njia mbadala ya serikali ya Muammar Qadhafi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amebaini kwa masikitiko na hofu kubwa kwamba helkopta tatu za kivita na vifaa vingine kutoka Belarus vimearifiwa kupelekwa Yamoussoukro kwa ajili ya majeshi ya Laurent Gbagbo.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM leo limeanza kuwasafirisha maelfu ya wahamiaji wanaokimbia machafuko nchini Afrika Kaskazini.
Umoja wa Mataifa umesema uko tayari kusaidia kipindi cha mpito cha kisiasa na kiuchumi nchini Misri.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Hilary Clinton akizungumza kwenye mkutano wa baraza la haki za binadamu amesema macho yote hii leo yanajikita kwa Libya.
Kamishina mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR Antonio Guterres ameelezea hofu yake juu ya maelfu ya wakimbizi na raia wa kigeni ambao huenda wamekwama nchini Libya.
Uongozi wa Libya umekosolewa vikali kutokana na ghasia zinazoendelea na ukandamizaji wa waandamanaji wanaipinga serikali.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limepiga kura kumuwekea vikwazo kiongozi wa Libya Muammar Qadhafi na kuitaka mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC kuchunguza uwezekano wa uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Juhudi za shirika la Umoja wa Mataifa la wakimbizi UNHCR pamoja na serikali za Burundi na Congo za kutaka wakimbizi wakongomani walioko Burundi kuanza kurudi nchini mwao kwa hiari zimegonga mwamba.