FAO inasaidia kuimarisha soko la mbegu Afrika
Mtandao wa Afrika wa kupima na kuzijaribu mbegu katika maabara FAST, umeanzishwa ili kuimarisha soko la mbegu za mazao mbalimbali barani humo.
Mtandao wa Afrika wa kupima na kuzijaribu mbegu katika maabara FAST, umeanzishwa ili kuimarisha soko la mbegu za mazao mbalimbali barani humo.
Mawaziri wa afya kutoka kote duniani leo wameanza mkutano wa siku mbili mjini Moscow Urusi ili kujadili magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Mwaka huu wa 2011 siku ya kimataifa ya usalama na afya kazini inajikita katika kutumia kama nyenzo mifumo ya utawala inayoshughulika na usalama na afya kazini ili kuendelea kuzuia matukio na ajali kazini.
Shirika la mpango wa chakula duniani WFP limesema linatiwa hofu na hali ya usalama wa chakula nchini Libya ambako kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa machafuko yamekuwa yakiendelea kwenye miji mbalimbali ikiwemo Tripoli, Misrata na Benghazi.
Wajumbe wa varaza la usalama leo wameafiki kuongeza muda wa mpango wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa ulioanzishwa wakati wa miwsho wa vita vya wenyewe kwa wenyewe baina ya Kusini na Kaskazini mwa Sudan na kuanzisha mpango mpya baada ya Sudan Kusini kujitenga rasmi mwezi Julai.
Timu ya wataalamu watatu wa Umoja wa Mataifa imewasili mjini Tripoli Libya kuchunguza madai ya ukiukaji wa haki za binadamu tangu kuanza kwa machafuko mwezi Februari mwaka huu.
Kikosi cha pamoja cha Umoja wa Mataifa na kile cha muungano wa Afrika cha kulinda amani kwenye jimbo la Darfur cha UNAMID kimeanzisha mPango wa kuhakikisha kuwa wenyeji wa jimbo hilo wamepata maji kwa njia rahisi.
Umoja wa Mataifa umesema kuwa takriban watu milioni 2.4 nchini Somalia wakiwa ni asilimia 32 ya watu wote nchini humo kwa sasa wanahitaji msaada wa kibinadamu lakini idadi hii huenda ikaongezeka zaidi kutoka na mzozo unaondelea kushuhudiwa nchini humo na ukame wa muda mrefu ambao umesababisha kufariki kwa mifugo wengi.
Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon ametaka kufanyika kwa uchunguzi kutokana na ghasia zinazoendelea nchini Syria baada ya vikosi vya serikali kuongeza matumizi ya nguvu dhidi ya waandamanaji nchini humo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amekaribisha kwa furaha hatua ya kuongezewa muda kamati iliyopewa jukumu la kufuatilizia azimio la umoja huo linalotaka kupigwa marafuku uzalishaji wa silaha za maangamizi.