08 Machi 2021
Hii leo Jumatatu Machi Nane ni siku ya wanawake duniani na jarida letu leo limejikita na siku hiyo tukimulika wanawake katika habari yetu kwa ufupi halikadhalika mashinani. Na kwa kuwa ni jumatatu, tuna mada kwa kina na leo tunakwenda nchini Tanzania kwake Ramlat Omar kijana wa kike ambaye anasimulia ni vipi amebadilika kutoka kuwa msichana hatarishi kwenye jamii yake hadi kuwa mkombozi na mjasiriamali wa kupita mlango hadi mlango kunusuru siyo tu vijana wa kike kama yeye bali pia wa kiume na vile vile wanawake kupitia mbinu alizopata kutoka shirika la kiraia la Restless Development.