Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

Juni 30 2021

Katika Jarida hii leo utasikia huko Paris nchini Ufaransa kumeanza jukwaa la siku tatu la kusaka kusongesha usawa wa kijinsia kwa kujumuisha vijana katika kufanikisha lengo hilo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ya Umoja wa Mataifa. Mkutano huo unafanyika kwa kuzingatia kuwa miaka 25 baada ya mkutano wa kimataifa wa wanawake huko Beijing nchini China, bado usawa wa jinsia unasalia ndoto kwa maeneo mengi.

Sauti
13'54"

Juni 29 2021

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema sasa taifa hilo lina wagonjwa zaidi ya 100 na tayari taratibu zinafanyika ili kuingiza chanjo ya COVID-19. Pia ameeleza tayari wameshajiunga na mpango wa Umoja wa Mataifa wa kuchagiza upatikanaji wa chanjo COVAX kwa nchi za kipato cha chini. 

Utapata pia kusikia namna mashirika ya Umoja wa Maifa yanavyosaidia kuinua maisha ya wananchi mashinani barani Afrika, mashirika hayo ni FAO,WFP pamoja na UNIDO.

Sauti
13'40"

JUNI 28 2021

Uchambuzi wa habari zetu hii leo ambapo kuelekea siku ya mabunge duniani juni 30 tutakuletea mahojiano maalum na mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Neema Lugangira kuhusu nafasi ya bunge kwa umma ikiwemo kuelimisha kuhusu mapambano ya Janga la CORONA. 

Pia utasikia habari kwa ufupi ambapo Flora Nducha atakujuza kuhusu ripoti ya UNODC, ubaguzi wa kimfumo na angalizo la WHO kuhusu akili bandia kwa afya. 

Juni 25 2021

Katika uchambuzi wa habari zetu hii leo Ijumaa  tutaelekea nchini Afghanistan kutazama namna mradi wa ukarabati wa mfereji wa umwagiliaji ulivyobadilisha maisha ya wananchi. Pia tutajifunza Kiswahili katika Neno la wiki, Dkt. Mwanahija Ali Juma Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar BAKIZA anafafanua maana ya msemo " IMANI YA DAKTARI. 

Sauti
10'19"

June 24, 2021

Katika Jarida hii leo utasikia Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la mpango wa chakula duniani WFP, David Beasley, ameiomba dunia kutoipa kisogo Masdagascar ambako maelfu ya watu wanakabiliwa na njaa kali na badala yake kujitoa na kuchukua hatua haraka baada ya kushuhudia mgogoro mkubwa usioonekana wa njaa unaoendelea Kusini mwa nchi hiyo  na kuathiri jamii nzima. 

Pia utasikia kuhusu wasiwasi wa wazazi nchini Palestina juu ya maisha ya baadae ya watoto wao ikiwa nchi yae itaendelea na machafuko. 

Sauti
12'11"

Juni 23 2021

Katika kufanikisha lengo la Muungano wa Afrika, AU kuhakikisha asilimia 60 ya wakazi wa bara lake wamepatiwa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 ifikapo mwaka 2022, Benki ya Dunia na AU wametangaza ubia wa kuunga mkono mpango wa kikosi kazi cha Afrika cha kupata chanjo hizo, AVATT utakaoruhusu nchi za Afrika kununua na kusambaza dozi za chanjo kwa ajli ya watu milioni 400 barani kote. 

Kwa habari hiyo na nyinginezo ikiwemo makala kutoka nchini Tanzania Bofya kusikiliza jarida letu la leo

Sauti
11'45"

Juni 22 2021

Katika Jarida la Habari za UN leo utasikia kuhusu Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo limezindua rasmi mwaka huu wa 2021 kuwa mwaka wa kimataifa wa wahudumu wa afya na wanaohudumia wagonjwa ikiwa ni kutambua mchango wao katika kukabiliana na ugonjwa wa Corona. Pia utasikia kuhusu ripoti ya hali ya watoto. 

Sauti
14'

21 Juni 2021

Leo katika Jarida Assumpta Massoi anakuletea

-Kamishina mkuu wa haki za binadamu Michelle Bachelet aitaka dunia kutoacha ukiukwaji wa haki za binadamu uendelee

-Shirika la afya la Umoja wa Msataifa WHO limesema milipuko ya Ebola Afrika Magharibi mwaka 2014-2016 imetoa funzo kubwa la kukabiliana na magonjwa na mchakato wa kusambaza chanjo

-Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO leo limetoa ripoti ya utafiti ikiangazia mifumo ya chakula ya watu wa asili na athari za kutoweka kwa mifumo hiyo kwa dunia katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi

Sauti
11'3"

18 JUNI 2021

Katika jarida la mada kwa kina la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea

-Mamilioni ya wakimbizi kuendelea kukabiliwa na njaa endapo msaada wa fedha za msaada hautopatikana limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP

-Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR imesema inatiwa wasiwasi miubwa na kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya raia na miundombinu yao kwenye jimbo la Marib nchini Yemen, mashambulizi yanayofanywa na kundi la Houthi

Sauti
13'3"

17 Juni 2021

Katika Jarida hii leo utasikia kuhusu Ujumbe wa Katibu Mkuu wa UN kuhusu kulinda Mazingira,  WHO yaonya ongezeko la wajawazito wanojifungua kwa njia ya Upasuaji, pia UNHCR inaendesha mkutano wa kujadili namna ya kuisaidia Venezuela

Sauti
12'45"