Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

30 NOVEMBA 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo miongoni mwa tuliyokuandalia hii leo ni pamoja na vipimo vya VVU vyapungua UNITAID  waomba ufadhili zaidi, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linatumia mabalozi wake watoto ambao ni wachechemuzi kuhusu tabianchi kuelezea adha ambazo watoto wanapata kutokana na madhara ya tabianchi na nini wanataka kifanyike.

Sauti
12'55"

29 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo jumatatu ni siku ya mada kwa kina na leo tunabisha hodi nchini Ghana kumulika adha za kukosa choo na jinsi Benki ya Dunia imeleta ahueni kwa familia husika kwenye mji mkuu wa taifa hio la Afrika Magharibi, ACCRA.

Pia utapata fursa ya kusikiliza habari kwa ufupi zikimulika masharti yaliyowekwa na Afrika kwa wanaotaka kutoa chanjo, kikao maalum cha WHO baada ya kutokea aina mpya ya kirusi pamoja na ujumbe wa Katibu Mkuu wa UN kwa siku ya mshikamano na watu wa palestina. 

Sauti
11'12"

26 Novemba 2021

karibu kusikiliza jarida ambapo leo tunabisha hodi Dubai kwenye maenesho ya kimataifa Expo2020 katika banda la Kenya kusikia kinachojiri huko na umuhimu wa Kenya kushiriki maonesho hayo.

Pia utapata fursa ya kusikia habari kwa ufupi zinazogusia mapigano huo Ethiopia na Sudan pamoja na upimaji binafsi wa VVU.

Sauti
10'56"

24 Novemba 2021

karibu kusikiliza jarida hii leo Flora Nducha anakuletea mada kwa kina maalum ikiwa ni kelele cha wiki ya kukuza uelewa kuhusu viuajiumbemaradhi, utasikia ushiriki wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula. 

Kabla ya mada hiyo kwa kina utasikia habari kwa ufupi zikiangazia masuala ya COVID-19 ambapo taarifa zinaonesha maambukizi yameendelea kuongezeka hususan barani ulaya lakini barani Afrika yamepungua. 

Pia utasikia kuhusu chanjo ya COVID-19 kwa watoto na Barubaru pamoja na wito uliotolewa kwa nchi zote duniani kuhusu usawa wa kijinsia. 

Sauti
12'33"

23 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida linaloletwa kwako na Flora Nducha ambapo hii leo nisiku ya furaha kwa wazungumzaji wa wa lugha ya Kiswahili kwani Umoja wa Mataifa umetangaza rasmi Julai 7 kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Kutokea nchini Kenya utakutana na Angela Andia mshindi wa mwaka 2021 wa mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF uitwao “wisdom project” au mradi wa busara ambao unashirikisha watoto wa umri wa kati ya miaka 9-14 kila mwaka wakishindana katika kuandaa Habari zinazohusua haki za mtoto.

Sauti
12'15"

22 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida leo tunajikita katika mada kwa kina kuangazia harakati za kusongesha viwanda vidogo vidogo barani Afrika hususan nchini Tanzania, kwa kuzingatia kuwa mwishoni mwa wiki ilikuwa ni siku ya viwanda barani Afrika.

Pia utapata fursa ya kusikiliza habari kwa ufupi

Sauti
11'41"

19 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo leo Flora Nducha anakuletea mada kwa kina ikijikita kuangalia changamoto zinazowakabili wakimbizi wa ndani ikiwemo huduma ya vyoo eneo la Uvira nchini DRC wakati dunia leo ikiadhimisha siku ya choo.

Sauti
10'50"

18 Novemba 2021

Hujambo na karibu kusikiliza jarida ambapo miongoni mwa ukayosikia leo ni pamoja na;- 

Kura ya maoni iliyoendeshwa katika nchi 21 ikihusisha watoto na watu wazima zaidi ya 21,000 imeonesha kuwa watoto wanaamini dunia inakuwa bora zaidi huku watu wazima wakiwa na shaka na shuku.

Mradi wa WFP kwa wakulima Zambia umekuwa neema Mkulima Mainner na familia yake.

Sauti
11'23"

17 Novemba 2021

Ni Jumatano ya tarehe 17 mwezi Novemba mwaka 2021 karibu kusikiliza jarida Assumpta Massoi anakuletea mada kwa kina maalum ikiangazia namna watoa huduma ya chakula wanavyojiimarisha kiuchumi na  kujikinga na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19

Pia utasikia muhtasari wa habari ikiwemo salamu za rambirambi kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenda kwa wananchi wa Uganda. 

Sauti
12'21"

16 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo leo Assumpta Massoi anakuletea habari mbalimbali ikiwemo mgogoro wa wananchi huko Cameroon baada ya kubuni mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la afya la Umoja wa Mataifa inaonyesha kwamba idadi ya watumiaji wa bidhaa za tumbaku duniani imepungua kwa zaidi ya watu milioni mbili.

Sauti
13'11"