26 Februari 2021
Leo Ijumaa ni mada kwa kina ikijikita huko jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako walinda amani wanawake kutoka Tanzania wakihudumu chini ya bendera ya Umoja wa Mataifa. Walinda amani hao chini ya TANZBATT_8 wamefanya ziara na kukutana na wanawake wa maeneo mbalimbali ikiwemo Matembo.