Juhudi za kimataifa za kuboresha maisha kwa wakazi wa mitaa ya mabanda Afrika Mashariki (Sehemu ya Pili)
Mwandishi habari wa Redio ya UM, Michele Montas hivi majuzi alizuru mtaa wa mabanda wa Mathare katika vitongoji vya Nairobi, mji mkuu wa Kenya.
Mwandishi habari wa Redio ya UM, Michele Montas hivi majuzi alizuru mtaa wa mabanda wa Mathare katika vitongoji vya Nairobi, mji mkuu wa Kenya.
Hivi karibuni, aliyekuwa mwandishi habari wa Idhaa ya Redio ya UM, Michele Montas alizuru Kenya kuangalia namna mashirika wenzi na UM yanavyoendeleza huduma za kupunguza umasikini, hasa miongoni mwa ule umma wenye kuishi kwenye mazingira ya hali duni.
Stephen Rapp, Mwendesha Mashitaka wa Mahakama Maalumu ya Sierra Leone juu ya Jinai ya Vita aliarifu wiki hii kuwa kesi ya aliyekuwa Raisi wa Liberia, Charles Taylor, inatazamiwa kuanza katika mji wa Hague, Uholanzi tarehe 04 Juni 2007. Taylor alifunguliwa mashitaka yenye kumtuhumu kuhusika na vitendo vilivyokiuka haki za kimsingi dhidi ya raia wa Sierra Leone wakati vita vya wenyewe kwa wenyewe viliposhtadi.
Mashirika sita ya UM, yakijumuika na Shirika lisio la kiserekali la kutoka Uholanzi lijulikanlo kama Baraza la Huduma za Wahamiaji la Kidachi,pamoja na jumuiya za kienyeji ziliopo katika mji wa bandari wa Bosaso, Usomali ya kaskazini wamejumuika kuhudumia mpango maalumu wa majaribio wenye lengo la kuzipatia aila 120 zilizong’olewa makwao baada ya mapigano kufumka, makazi mapya. Vile vile familia 30 nyengine masikini kutoka eneo la Bosaso nazo zitafadhiliwa makazi.
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeshtumu vikali utekaji nyara na mashambulio yaliyofanyika mwisho wa wiki iliopita, dhidi ya misafara ya magari matupu 48 yaliokuwa yakirejea katika mji wa Khufra, Libya ya kusini kutokea Chad ya Mashariki. Haya ni mashambulio ya tatu dhidi ya misafara ya WFP katika miezi miwili iliopita.
Bodi la Utendaji la Shirika la Afya Duniani (WHO), ambalo hukutana mara mbili kwa mwaka, Ijumatatu lilianza mjini Geneva kikao cha awali kwa 2007. Katika hotuba ya ufunguzi, Mkurugenzi Mpya wa WHO, Dktr Margaret Chan alizungumzia mafanikio yaliojiri karibuni katika kuboresha afya ya jamii.
KM Ban Ki-moon alianza ziara rasmi Ijumanne kuyatembelea mataifa saba ya Ulaya na Afrika. Hii ni ziara kuu ya kwanza ya KM tangu alipochukua madaraka ya kuuongoza UM Janauari mosi.
Louise Arbour, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Utekelezaji wa Haki za Kibinadamu Ulimwenguni alinakiliwa akisema kuna ulazima wa tume huru kubuniwa itakayoendeleza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji yaliotukia 10 Januari 2007 kufuatia mgomo wataifa ulioaznishwa wakati huo.
Mapema wiki hii KM Ban aliripoti kuingiwa wasiwasi kuhusu athari za operesheni za Serekali ya Sudan katika Darfur Kaskazini, ambako inasemekena ndege zake za kijeshi zilishambulia hivi karibuni raia na kujeruhi idadi kubwa yao.
Mjumbe Maalumu wa UM juu ya Hifadhi ya Watoto kwenye Mazingira ya Uhasama na Vita, Radhika Coomaraswamy anatazamiwa kuzuru Sudan mwisho wa wiki kwa kuitikia mwaliko wa Serekali ya Sudan.