Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kesi ya Charles Taylor kuanza mwanzo wa Juni mjini Hague

Kesi ya Charles Taylor kuanza mwanzo wa Juni mjini Hague

Stephen Rapp, Mwendesha Mashitaka wa Mahakama Maalumu ya Sierra Leone juu ya Jinai ya Vita aliarifu wiki hii kuwa kesi ya aliyekuwa Raisi wa Liberia, Charles Taylor, inatazamiwa kuanza katika mji wa Hague, Uholanzi tarehe 04 Juni 2007. Taylor alifunguliwa mashitaka yenye kumtuhumu kuhusika na vitendo vilivyokiuka haki za kimsingi dhidi ya raia wa Sierra Leone wakati vita vya wenyewe kwa wenyewe viliposhtadi.