Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP yashtumu mashambulio dhidi ya misfara yake nchini Chad

WFP yashtumu mashambulio dhidi ya misfara yake nchini Chad

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeshtumu vikali utekaji nyara na mashambulio yaliyofanyika mwisho wa wiki iliopita, dhidi ya misafara ya magari matupu 48 yaliokuwa yakirejea katika mji wa Khufra, Libya ya kusini kutokea Chad ya Mashariki. Haya ni mashambulio ya tatu dhidi ya misafara ya WFP katika miezi miwili iliopita.