Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Umma ulion'golewa mastakimu Usomali kupatiwa makazi mapya

Umma ulion'golewa mastakimu Usomali kupatiwa makazi mapya

Mashirika sita ya UM, yakijumuika na Shirika lisio la kiserekali la kutoka Uholanzi lijulikanlo kama Baraza la Huduma za Wahamiaji la Kidachi,pamoja na jumuiya za kienyeji ziliopo katika mji wa bandari wa Bosaso, Usomali ya kaskazini wamejumuika kuhudumia mpango maalumu wa majaribio wenye lengo la kuzipatia aila 120 zilizong’olewa makwao baada ya mapigano kufumka, makazi mapya. Vile vile familia 30 nyengine masikini kutoka eneo la Bosaso nazo zitafadhiliwa makazi.